IMG-20140107-WA0007
Pichani ni magari ya kuzolea taka ngumu ya kampuni mbalimbali yakiwa kwenye foleni ya kuingia Dampo la Pugu Kinyamwezi ambalo miundo mbinu yake ni mibovu na kupelekea zoezi hilo kuchukua zaidi ya siku 4 mpaka kufanikisha kufikia eneo maalum la kumwagia taka ngumu.
.Ni kutokana na kukwama kwa magari ya taka kwenye Dampo la Pugu
.Siku ya tatu sasa magari ya taka yamekwama

Na. Mwandishi wetu,

MIUNDOMBINU mibovu katika Dampo kuu la jiji la Dar es Salaam Pugu Kinyamwezi imesababisha magari makubwa ya kuzoa na kumwaga taka kukwama kwa muda wa siku tatu na kupunguza ufanisi wa kuzoa taka katika mkoa wa Dar es Salaam.

Mtoa taarifa wetu ambaye hakutaka kutajwa kwenye blogu hii, amesema kwamba uongozi wa Dampo Pugu umeshidwa kuweka utaratibu mzuri na kukarabati miundombinu ya dampo kwa muda mrefu na kusababisha msongamano mkubwa wakati wa kwenda kumwaga taka katika sehemu hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. TUNASUBIRI MZUNGU AJE ATUSAIDIE

    ReplyDelete
  2. Uzuri wanasoma Michuzi; hivyo wameona (wazungu) watakuja kutoa msaada!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...