Makamu Mwenyekiti wa CCM,Phillip Mangula akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum, Dk. Mary Mwanjelwa baada ya kuwasili leo asubuhi kwenye Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya , tayari akwa maadhimisho ya miaka 37 ya CCM yatakayofanyika kitaifa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, jijini Mbeya Jumapili Februari 2. Kushoto ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.
 Mangula (katikati) akiwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye (kulia) pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya, Godfrey Zambi.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (katikati) akizungumza na Nape (kulia) pamoja na Zambi kwenye chumba cha watu mashuhuri (VIP) alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe, Mbeya leo mchana, tayari kwa maadhimisho hayo.
 Nape (kulia) akizungumza na Kinana pamoja na Zambi kwenye Uwanja wa Ndege wa Songwe
Dk. Mary Mwanjelwa (kushoto) akijadiliana jambo na Makmu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Dogo Idd Mabrouk wakati wa mapokezi hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Mh. Nape punguza uzito kaka, unakoelekea si kuzuri kwa afya yako.

    Ni ushauri tu.

    ReplyDelete
  2. Sawa, Waheshimiwa Kinana, Zambi na Nnauye mmnasemaje kuhusu Kichwa cha Habari ktk uso wa Gazeti la leo la MWANANCHI analosoma Mhe. Nape Nnauye?

    Huu ndio wakati wa kumfunga paka Kengele!

    Nani atamkata Mkia Simba?

    Ujenzi wa Chama cha Mapinduzi kazi tunayo!

    ReplyDelete
  3. Kazi ipo Mbeya, kwa kuwa Magwandazzz yameshamiri sana nafikiri Wanyampala ndugu zetu wamechukulia lile baridi la kule kwao na Msaada wa Chama wa MAKOTI YA KAKHI kama ndio njia ya kulikabili baridi!!!

    ReplyDelete
  4. Nadhani Wandugu zetu Mbeya meshuhudia ubovu wa Kyadema na fukuza fukuza kiholela za wanachama!

    Huu ndio wakati wa kuvua Magwandazzz!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...