
Mbunge wa jimbo la Iringa Mjini,Mh.Peter Msingwa amefanya mkutano hapo jana katika viwanja vya Mwembetogwa, mkoani humo.
Mkutano huo ambao ulikuwa wa kufungia mwaka 2013 ,Msigwa pia aliutumia mkutano huo kwa kuwapongeza baadhi ya mawaziri ambao utendaji kazi wao unaonekana kuwa mzuri,akiwemo Waziri wa Wizara ya Maji na Naibu Wake ,Waziri wa Ujenzi na Waziri wa Mazingira ambao wameonesha msimamo wa kweli katika kuwatumikia wananchi .
katika hatua nyingine mbunge Msigwa amemshukia aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema,Zitto Kabwe na kusema kuwa anatafuta umaarufu binafsi kuliko kukijenga chama chake na kuwa hana nia njema na CHADEMA,hivyo amewataka Wanachadema wa jimbo la Iringa mjini kutomsikiliza huku akibainisha kuwa Mwanachama na Kiongozi mzuri ni yule ambae anafanya kazi ya kukijenga chama chake na si kujijenga yeye binafsi.
Amesema kuwa iwapo Zitto hatotaka kumsikiliza mwasisi wa Chama hicho, Mzee Mtei wala kuwasikiliza viongozi wa juu wa chama hicho akiwemo mwenyekiti wa katibu mkuu, ni wazi hakitakii mema CHADEMA,na wana Chadema hawana budi kumpuuza kiongozi na mwanachama yeyote mwenye lengo la kuua chama.
Kuhusu rasimu ya Katiba, Mbunge Msigwa amempongeza Rais Kikwete kuwa ameonyesha ushujaa wa hali ya juu katika kupigania upatikanaji wa katiba mpya, na kuwa iwapo wabunge wa CCM watapinga wao kama Chadema watarudi kwa wananchi kuhamasisha kupiga kura ya kuikataa katiba itakayopendekezwa na wabunge wa CCM.
Aidha Msigwa ameongeza kusema kuwa atakuwa mstari wa mbele kuikosoa serikali kama itaonekana kuwa na viongozi dhaifu huku akiwataka watanzania kutathimini yale yote waliyofanya mwaka 2013 na kuwatakia kheri ya mwaka mpya.


Watakutimua wenyewe, ukakosa ulaji, shauri yako, we sifia tu!
ReplyDeleteTayari huyu Mhe.ameanza kujifunza siasa.Si kila kitu kinachotoka upande wa pili yaani kwa Serikali au chama tawala ni kibaya. Lazima tuonyeshe ubora wa siasa zetu za ndani na ukomavu. Na kama alivyosema mchangiaji wa kw3anza mabosi wake huyu Mhe.si dahni kama wataifurahii kauli sahihi aliyoitoa kwani wao ni vita tu kila kitu.
ReplyDeleteSiasa za Tanzania zinaanza kukomaa.Naushabihi mtizamo wa Mh.Msigwa;kwamba JK katutendea jambo jema kwa kuleta wazo la kurekebisha Katiba ya Tanzania.Pia natoa hi kwa msimamo wa Mh J.Mbatia kwa msimamo wake wa Taifa Kwanza.Ni kheri viongozi wa CHADEMA waanze kuliona hili pia;ikiwa wanataka kushika dola 2015.Mh.Mwigulu hafai hata ndani ya CCM;ukomunisti na uhafidhina ni UZAMANI;ATOSWE na CCM,atoswe na JK pia.Sasa waTz tunataka amani na sisa safi.Basi.
ReplyDelete