Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL unawatangazia
abiria wote na wananchi kwa jumla kuwa
kutokana na sababu za kiufundi unasikitika kuwa treni ya abiria iliyopangwa
kuondoka leo Alhamisi Januari 09, 2014 saa 3 usiku kwenda bara imeahirishwa
hadi kesho siku ya Ijumaa Januari 10, 2014, saa 10 jioni.
Taarifa imefafanua kuwa dharura hiyo imetokana na eneo la
reli kati ya stesheni za Godegode na
Gulwe mkoani Dodoma kukumbwa na mafuriko
usiku wa kuamkia leo.
Wahandisi na Mafundi wa TRL wako katika eneo la tukio
tokea jana usiku na taarifa za uhakika
zinaeleza kuwa zoezi la kukarabati
litakamilika saa 10 leo jioni ( Alhamis Januari 09, 2014).
Aidha taarifa hii
iwafikie wadau wote wa usafiri na huduma ya reli ya kati na kwamba uongozi wa
TRL unaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza..
Imetolewa
na Ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Mhandisi Paschal
Mafikiri.
TRL Makao
Makuu,
Dar es
Salaam.
Januari 09,
2014
SIJUI LINI UMASIKINI HUU UTAKWISHA, MANAKE TUKO ENZI ZA UJIMA BADO
ReplyDeleteBasi watume za mizigo jamaniiiii ah
ReplyDeletena nyie kampuni ya reli wakati umefika, mbadilike sasa. abiria wakija kukata tiketi chukueni na namba zao za simu ili kama kuna mabadiliko muwajulishe, mtu anatoka mbali kuja rly stesheni anakuta imeahirishwa kwa siku hiyo, na vichapati vyake na watoto, ni usumbufu kweli!!! kuna kabang, airtel yatosha, cheka time ...., jiungeni mtume messages kwa abiria wenu. bado mko zama za kale tu! ndo maana hata wafanyakazi wenu wachovu sana hawana hata maendeleo.
ReplyDelete