Wananchi mbalimbali wakipata maelezo ya kina juu ya umuhimu wa taarifa za hali ya hewa katika banda la TMA kwenye maonesho ya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Meneja Kituo cha Zanzibar Bw. Said Khamis akimwelezea mwananchi njia mbalimbali za ukusanyaji wa takwimu za hali ya hewa kwenye maonesho ya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Ofisa Uhusiano wa TMA Bi.Monica Mutoni akitoa elimu kwa umma jinsi ya kupata taarifa za hali ya hewa kupitia njia mbalimbali za usambazaji wa taarifa hizo kwenye maonesho ya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Mkurugenzi wa ofisi ya Zanzibar, Bw Mohamed Ngwali akitoa maelezo ya takwimu za hali mbaya ya hewa iliyowahi kutokea kwa kipindi cha miaka 50 katika visiwa vya Unguja na Pemba, akisisitiza wananchi kutopuuza tahadhari zitolewazo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...