Na Mwenekaya Said,Globu ya Jamii - Kisutu 

KESI  ya  mauaji ya kukusudia  inayomkabili Mfanyabiashara maarufu nchini,Marijan Abubakar maarufu kama Papa Msofe (50) na mwenzake Makongoro Joseph Nyerere katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, bado inafanyiwa kazi  kwa Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) kwa ajili ya hatua zaidi.

Kesi hiyo imeahirishwa leo, na Hakimu Mkazi Hallen Riwa amesema kwa kuwa jalada la kesi liko kwa DPP na kwamba washtakiwa wanatakiwa kuwa na subira.

Hakimu Riwa alisema  kesi hiyo ilitajwa Februari 25, mwaka huu  kwa ajili ya kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.

Kabla ya kupanga tarehe hiyo, mshtakiwa wa pili Makongoro aliulalamikia upande wa Jamhuri kuwa unachelewesha upelelezi wa kesi yao kwa makusudi na kwamba wao wamekaa muda mrefu gerezani wanateseka.

Msofe ambaye kwa mara ya kwanza alifikishwa mahakamani hapo Agosti 10, mwaka 2012  anadaiwa kuwa yeye pamoja na mwenzake  Makongoro, Novemba 6,  mwaka 2011  huko Magomeni Mapipa kwa kukusudia walimuua Onesphory Kitoli.

Ilidaiwa kuwa washtakiwa hao walifanya kosa hilo kinyume na kifungu cha 196 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka ya mwaka 2002.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Jela kumempenda jamaa; naona ametoka mchicha haswa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...