Mjumbe wa Bunge la Katiba na Mwenyekiti wa Timu ya Simba Ismail Aden Rage akiwaonyesha wajumbe wa Bunge hilo Kadi ya ATM kupitia Benki ya Posta inayotumiwa na wanachama wa Simba. Wengine ni Richard Ndasa(kulia), Khalifa Suleman Khalifa (wa pili kushoto) naMurtaza Mangunga(kushoto).
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Thomas Kashililah (kushoto) akibadilishana mawazo na Mjumbe wa Bunge la Katiba William Lukuvi(kulia) .
Mjumbe wa Bunge la Katiba Joshua Nasari(kulia) akibadlishana mawazo na Afisa Habari wa Bunge la Jamhuri Owen Mwandumbya(kushoto) kwenye viwanja vya Bunge jana mjini Dodoma.
Mjumbe wa Bunge la Katiba Ismail Aden Rage( wa pili kulia) akibadlishana mawazo na Afisa Habari wa Bunge la Jamhuri Owen Mwandumbya(kulia), Mtangazaji wa Mlimani TV Egbert Mkoko(kushoto) na Mpiga picha wa Mlimani TV Hayqal Mushi jana mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. The mdudu,mm nashindwa kuelewa mtu kwenye timu tu ya mpira anashindwa kuweka mambo sawa kama vile kuwa na mawazo ya kujenga uwanja wa kisasa yanamshindwa je huko kwenye bunge la katiba atachangia nini? Amakweli kukaa kwangu huku nimejifunza mengi sn poleni sn na maisha yenu ya zurumati zurumati kwa umaa wa watanzania lakini kesho kwa mungu mtatia akili

    ReplyDelete
  2. HIVI HILI BUNGE HALINA DRESS CODE?

    ReplyDelete
  3. Kweli sie wajinga ndio tuliwao! Nikitazama picha zote isipokuwa ya Mhe. Lukuvi na mwenzake ndio angalau inaonyesha kwamba watu wapo makini na kilicho mbele yao. Nyingine zote zinaonyesha wapo hapo kufanya maonesho na kudai maslahi ya matumbo yao. Naomba niwakumbushe ipo siku tutawachokoka na cha mtema kuni mtakiona.

    ReplyDelete
  4. Ankal, Mwambie RAge Simba wanasoma halbadiri

    ReplyDelete
  5. aise kweli kabisa, haya mambo ya tisheti na jinzi wapi na wapi??

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...