Zile habari zilizosambaa kwenye mitandao  ya kijamii  kuonesha  kwamba hotel ya Naura Spring ya jijini Arusha inawaka moto zilikuwa si za kweli ni watu wametengeza picha hizo ambazo zilikuwa zimeenea kila pembe.
Kamanda wa Polisi Arusha Liberatus Sabas ameongea jioni hii na vyombo vya habari na kukanusha habari za hotel hiyo ya kitalii jijini Arusha kwamba iliwaka moto hizo ni picha za kutengeneza hotel ipo salama kabisa kama unavyoona kwenye picha ya juu. Picha ya chini yake ndiyo iliyosambazwa na watu wasiojulikana.  
Wananchi wengi wamepiga simu dawati la usiku la Globu ya Jamii na kueleza masikitiko yao kwa mchezo huu unaoenea kwa kasi nchini hivi sasa. Wamevitaka vyombo husika sio tu kudhibiti uhalifu huu bali pia kuwachukulia hatua watakaobainika kuhusika nao. 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Liberatus Sabas  ambaye amekanusha kwamba  Naura Springs Hotel imewaka moto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 19, 2014

    Mambo gani haya ya kuzusha habari ambazo hazikutokea???

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...