Na Andrew Chale
TAASISI ya  Mwangaza wa buradani Zanzibar  (Zanzibar Light Entertainment ) ya mjini Unguja,  Zanzibar, Imemtangaza rasmi  Hotel ya Kendwa Rocks  kuwa eneo litakapofanyika  michuano m aalum ya soka la ufukweni  lijulikanayo kama  (Zanzibar Beach Soccer Championship Bonanza) linalotarajiwa kufanyika Agosti  Mbili mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa yao hiyo  kwa vyombo vya habari, iliyotolewa na Mwandaaji wa michezo hiyo, Muslim Nassor ‘Jazzphaa’  ilieleza kuwa,  kamati ya mashindano hayo, ambayo kwa sasa hipo katika harakati mbalimbali zikiwemo za kusaka ufadhili kwa wadau, tayari baadhi ya wadau wameanza kuitikia wito huo huku Kendwa Rocks Hotel Beach, wakijitosa kudhamini ‘venue’.

“Kadri siku zinavyozidi kwenda ndipo maandalizi yanakuwa magumu zaidi. Tunafuraha kutoa taarifah kuwa ndipo tutakapofanyia mashindano haya ya Zanzibar Beach Soccer Bonanza 2014.” Alisema Muslim Nassor  Jazziphaa.

Aidha, Muslim Nassor Jazziphaa aliweka bayaana kuwa,  Director wa Kendwa rocks, Bwana Ally Kilupi  tayari ametoa   baraka  zote za kufaanyika mchezo huo huku akifurahia mchezo kufanyika eneo hilo,  huku akitoa rai kuwapo kwa amani na utulivu siku hiyo na siyo kuanza ugomvi na vitu ambavyo havina maana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...