Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Comoro,Mhe. Chabaka Kilumanga ameshiriki katika shughuli ya kuwakumbuka wahanga wa mashambulizi ya kigaidi yaliyofanywa katika Ofisi za Charlie Hebdo, jijini Paris, Ufaransa. Shughuli hiyo, iliyoandaliwa na Balozi wa Ufaransa nchini Comoro na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali ya Comoro, Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa pamoja na watu mashuhuri, iliambatana na kusaini kitabu cha maombolezi.
Mhe. Balozi Chabaka Kilumanga akisalimiana na Mhe. Ahmed Abdallah Mohamed Sambi, wakati akiwasili katika maombolezi ya mashambulizi ya Charlie Hebdo.
Mhe. Balozi Chabaka Kilumanga akisaini Kitabu cha Maombolezi ya Wahanga wa Mashambulizi ya Charlie Hebdo. Kushoto, aliyesimama ni Balozi wa Ufaransa nchini Comoro.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Angalao pia watie saini kitabu cha maombolezo kwa wahanga wa Nigeria ambao melfu wameisha uwawa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...