Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wakurugenzi wa Chama cha Ushirika cha Ujenzi wa Nyumba Mwenge (MHCS Ltd), Hillaly Mdaki akizungumza wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo, uliofanyika Afrika Sana Mwenge jijini Dar es Salaam.Kulia ni makamu mwenyekiti wa bodi hiyo, Hellena Khamsini.
Mjumbe mmojawapo wa bodi ya hiyo, Ndesumbuka Merinyo akisaini hati ya kiapo cha kuitumikia nafasi hiyo katika hafla iliyofanyika Sinza, Afrika Sana jana.


Bodi Mpya ya Wakurugenzi wa Chama cha Ushirika cha Ujenzi wa Nyumba Mwenge (MHCS Ltd), imezinduliwa rasmi jana ambayo pamoja na mambo mengine, imejizatiti kuhakikisha inatekeleza miradi ya maendeleo kwa ajili ya wanachama wake.

Akizungumza mara baada ya kuapishwa, mwenyekiti wa bodi hiyo Hillaly Mdaki alisema kuwa pamoja na mambo mengine itahakikisha inatekeleza miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na ile ya ujenzi wa majengo pacha yenye urefu wa ghorofa 32 katika kiwanja ilipo Afrika Sana, Sinza jijini Dar es Salaam.

Pia ujenzi wa nyumba za wanachama na vitegauchumi vingine kupitia mikopo ya mabenki katika eneo la kiwanja chenye ukubwa wa ekari 800 katika eneo la Kibiki, Chalinze mkoa wa Pwani. Mdaki alisema serikali kupitia mrajisi wa vyama vya ushirika imewakabidhi eneo hilo Chalinze na wanachama 378 tayari wamekabidhiwa viwanja na hati za umiliki wa viwanja hivyo na awali waliomba Bagamoyo lakini wakapatiwa Chalinze, jambo ambalo alisema ni jema.

“Lengo ni kuhakikisha wanachama ambao wengi wao ni wastaafu wa serikali wananufaika na ushirika” alisema na kuongeza kuwa bodi iliyozinduliwa pamoja na mambo mengine ina jukumu la kuhakikisha ujenzi wa nyumba hizo za wanchama unakamilika na kupitia mikopo ya mabenki.

“Pia bodi ina jukumu la kuhakikisha mradi wa majengo pacha yatakayokuwa na jumla ya ghorofa 32 ikiwa ni idadi ya 16 kila upande unakamilika” alisema na kuongeza kuwa michoro kwa ajili ya ujenzi huo imekamilika.

Alibainisha kuwa majengo hayo pacha yatajengwa katika kiwanja hicho ilipo Afrika Sana, eneo ambalo walipewa na Rais wa Awamu ya Kwanza, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1971 na pia wamelenga kutekeleza miradi kadhaa ya ujenzi mikoani pia.

Tupo Mwenge ambayo ni alama ya mwangaza kwa nchi nzima hivyo nasi tutatekeleza miradi hiyo ya ujenzi katika mikoa mingine 10 nchini kwa kuanzia lengo kufanya hivyo nchi nzima” alisema na kuongeza kuwa viwanja 77 vitagawiwa kwa wakazi wengine wa jiji ambao watahitaji.

Awali mwenyekiti anayemaliza muda wake, aliwataka wajumbe na mwenyekiti mpya kufanyakazi kwa kufuata kanuni, sheria ya vyama vya ushirika na katiba na alibainisha kuwa hadi kufikia ulipo huo ushirika ni jitihada binafsi za wanachama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Sasa nimeelewa historia ya Afrika Sana, Sinza Mwenge jijini Dar-es-Salaam na influence ya Baba wa Taifa juu ya dhana ya Ujamaa na Kujitegemea kama hawa Wanachama wanavyojipanga kujitegemea kwa vitendo.

    Hongereni sana.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...