Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.
WAKALA wa
usajili ufilisi na udhamini(RITA) wamewataka wazazi na walezi wanaosoma shule
za msingi za Manispaa ya Kinondoni wawaandikishe watoto wao ili waweze kupata
vyeti vyao vya kuzaliwa.
Hayo
yamesemwa na Meneja masoko Mawasiliano na Elimu kwa Umma wa RITA Josephat Kimaro
wakati akizungumza na wandishi wa habari
katika ukumbi wa Habari MAELEZO leo jijini Dar es Salaam.
Kimaro amesema
kuwa wananchi wajue umhimu wa cheti cha kuzaliwa kwani Cheti cha kuzaliwa ni
nyaraka inayodhibitisha taarifa muhimu za wananchi ikiwa ni pamoja na tarehe ya kuzaliwa, mahali alipozaliwa, wazazi halisi na miliki halali wa cheti.
Pia Kimaro
amesema kuwa kila shule ya msingi ya Manispaa
ya Kinondoni wameteua Mwalimu mmoja ili
kuhakikisha kila Mwanafunzi anapewa cheti cha kuzaliwa.
Amesema kuwa
zoezi la uandikishaji wa wanafunzi wa
shule za msingi katika Manispaa ya Kinondoni, walioomba na waliopewa vyeti
katika shule hizo ni wanafunzi 5081 kati ya hao ni wasichana 2720 na wavulana
2361.
Meneja masoko Mawasiliano na Elimu kwa Umma wa RITA Josephat Kimaro akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani katika ukumbi wa habari MAELEZO jijini Dar es Salaam leo, kulia ni Msajili wa vizazi na vifo Mariam Ling'ande.
Msajili wa vizazi na vifo Mariam Ling'ande akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,kushoto ni Meneja masoko Mawasiliano na Elimu kwa Umma wa RITA Josephat Kimaro.
Baadhi ya wandishi wa habari waliohudhulia katika mkutano na
Wakala wa usajili ufilisi na udhamini(RITA) jijini Dar es Salaam leo.(PICHA NA EMMENUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII)
Wakala wa usajili ufilisi na udhamini(RITA) jijini Dar es Salaam leo.(PICHA NA EMMENUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...