KWAYA ya Uinjilisti ya Kijitonyama imechomoza kumsindikiza mwimbaji nguli wa muziki wa Injili Tanzania Bonny Mwaitege anayetarajia kuzindua albamu tatu, uzinduzi unaotarajia kufanyika Agosti 2 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
 
Sambamba na Kwaya hiyo  pia uzinduzi huo utasindikizwa na mwimbaji mwingine mahiri Afrika Mashriki na Kati, Joshua Mlelwa ambaye ni machachari zaidi awapo jukwaani.
 
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama  uzinduzi huo unatarajia kusindikizwa na waimbaji mbalimbali wa Tanzania na nje lengo likiwa ni kufanikisha uzinduzi mahiri wa albamu hizo.
 
Msama alisema pamoja na uzinduzi huo kusindikizwa na waimbaji mahiri pia, waimbaji chipukizi watamsindikiza Mwaitege ambaye hivi sasa anaendelea na mazoezi kuelekea uzinduzi huo.
 
Aidha Msama alisema hivi sasa muimbaji huyo pia anamalizia kurekodi baadhi ya nyimbo zilizomo kwenye albamu hizo katika majiji ya Mwanza, Arusha, Mbeya  na Nairobi.Msama alisema uzinduzi huo baada ya kufanyika Dar es Salaam, Agosti nane utahamia Wilayani Makambako mkoani Njombe na siku inayofuata watazindua albamu hizo kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
 
msama alitumia fursa hiyo kutoa wito kwa mashabiki wa muziki wa injili kujiandaa na uzinduzi huo ambao utakuwa ni wa aina yake."Maandalizi makubwa kuelekea uzindizu wa Mwaitege yameshafanyika, kilicho mbele ni uzinduzi wa hali ya juu, mashabiki wakae mkao wa kula," alisema Msama na kuongeza.
 
"Uzinduzi wa Mwaitege utakuwa ni wa aina yake kwa sababu maandalizi yake kwa sababu yamefanywa kwa ustadi mkubwa, mashabiki watarajie kazi bora zaidi kutoka kwa muimbaji huyo," alisema.  
 
Bonny Mwaitege anatamba na nyimbo mbalimbali kama Mama ni Mama, Mke mwema, Wakusamehe, Fungua Moyo wako, Njoo  uombewe na  Yesu yupo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...