Mkuu wa Masoko na Mauzo wa Vodacom Tanzania kanda ya ziwa,Dominician Mkama(wa kwanza kushoto) akishirikiana na baadhi ya wafanyakazi wenzake kukata utepe kuashiria uzinduzi wa duka la kampuni hiyo mkoani mwanza baada ya kukarabatiwa upya katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika mwishoni mwa wiki.
 Baadhi ya wateja wa Vodacom Tanzania kanda ya ziwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo wakigonganisha glasi kufurahia uzinduzi wa duka la kampuni hiyo upya baada ya kukarabatiwa kwa muda wa miezi miwili jijini Mwanza.
 Mteja wa Vodacom Tanzania kanda ya ziwa,Farida Omar (kushoto)akilishwa keki na Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kanda ya ziwa wa kampuni hiyo,Dominician Mkama(kulia)wakati wa uzinduzi wa duka la kampuni hiyo upya baada ya kukarabatiwa kwa muda ya miezi miwili jijini Mwanza.
Mteja wa Vodacom Tanzania kanda ya ziwa,John Mwaseka (kushoto)akilishwa keki na Mkuu wa Masoko na Mauzo wa kanda ya ziwa wa kampuni hiyo,Dominician Mkama(kulia)wakati wa uzinduzi wa duka la kampuni hiyo upya baada ya kukarabatiwa kwa muda ya miezi miwili jijini Mwanza.
 Baadhi ya wakazi wa jiji la Mwanza wakipatiwa huduma mbalimbali za mawasiliano kwenye duka la Vodacom Tanzania mkoani humo mwishoni mwa wiki baada ya duka hilo kuzinduliwa upya baada ya kukarabatiwa kwa muda wa miezi miwili.
Hili ndilo duka jipya la Vodacom Tanzania mkoani mwanza mara baada ya kukarabatiwa upya,hafla ya uzinduzi wake ilifanyika hivi karibuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...