Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kushoto) akimsalimia Mkuu wa Jeshi la Magereza, Kamishna Jenerali (CGP), John Minja wakati alipokuwa anawasili ofisi ya Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya ziara ya kikazi. Katibu Mkuu Rwegasira alilipongeza jeshi hilo kwa utendaji wa kazi mzuri licha ya kuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali. Kulia ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi hilo, Gaston Sanga, na anayefuata ni Kamishna wa Sheria na Utawala wa Jeshi hilo, Dk Juma Malewa.
Mkuu wa Jeshi la Magereza, Kamishna Jenerali (CGP), John Minja akitoa taarifa ya utendaji wa Jeshi lake kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (katikati meza kuu) wakati Katibu Mkuu huyo alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam. Katibu Mkuu Rwegasira alilipongeza jeshi hilo kwa utendaji wa kazi mzuri licha ya kuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali. Kushoto meza kuu ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Simba Yahya.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (katikati) akizungumza na Makamanda wa Jeshi la Magereza wakiongozwa na Kamishna Jenerali, John Minja (kushoto meza kuu) wakati Katibu Mkuu na Naibu wake walipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam leo. Katika hotuba yake, Meja Jenerali Rwegasira alilipongeza jeshi hilo kwa utendaji wa kazi mzuri licha ya kuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Simba Yahya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...