Na  Bashir  Yakub .

Kupitia  makala  haya  wako  Watanzania ambao wanao  marafiki  wa  kigeni, wanao wafanyabiashara  wenzao  wa  kigeni,  ndugu  wa  kigeni, na  wengine  wanahisa  wenzao  katika  makampuni  mbalimbali  ambao  wangependa   wenzao   hao  wapate  ardhi  ya  uwekezaji  Tanzania.  Makala  haya  ni  nafasi  kwao  kujua  mambo  ya  msingi  ya  awali  kuhusu  namna  ya  kupata  ardhi   kwa  hao  wageni.

Aidha mara  kadhaa  makala  yetu  yameeleza   taratibu  mbalimbali  ambazo   Mtanzania  huweza  kupitia  ili  kupata  haki  ya  kumiliki  ardhi. Sanjari  na  hilo   imeelezwa  mara nyingi pia  namna  nzuri  ya kuweza   kupata  ardhi  huku  ukiepuka  migogoro  ambayo  huwaingiza  wengi  katika  hasara  ikiwa  ni  pamoja  na  kuwapotezea  muda. 

 Iliwahi  kuelezwa  hapa  kuwa  Mtanzania  anaweza kupata ardhi  kwa  kununua,  kurithi, kuzawadiwa,  njia ya  fidia,  na kwa  kutwaa  eneo  lisilo  na  mmiliki.     

Hii ni  kwa raia  wa  Tanzania.  Yumkini raia    wasio  watanzania  nao  wanazo  haki  zao  katika   ardhi  yetu. Raia  wasio  Watanzania  wanaweza  kupatiwa  ardhi  kwa ajili  ya  matumizi. Kubwa  kwao  hupatiwa ardhi  kwa  ajili  ya  uwekezaji   kwa  manufaa  ya  taifa. 

 Kupitia  hili  zipo  namna  tano  ambazo  raia wasio  Watanzania  wanaweza  kupitia  hadi kupatiwa  ardhi.

1.SHERIA  ZINAZOWARUHUSU  WAGENI  KUPATIWA  ARDHI.
Sheria  kuu  inayowaruhusu  raia  wa  kigeni  kupatiwa  ardhi nchini  ni  sheria  namba  4   sheria  ya  ardhi  ya  mwaka  1999.  Kifungu  cha  19( 2 )  cha  sheria  hii  kinasema  kuwa  mtu  au  kikundi  cha  watu  ambacho  kimejiunga  kama  kampuni  au   bila  kampuni  ambacho  wahusika  wake  ni  raia  wa  kigeni  wanaweza  kupata  haki  ya  kumiliki  ardhi  kwa  ajili  ya  uwekezaji. 

Sheria  nyingine   inayotoa  mwongozo   kwa  raia  wa  kigeni  kupata ardhi  Tanzania  ni   sura  ya  38 sheria  ya   uwekezaji  ya  mwaka  1997. Sheria    hii  hueleza  namna  ya  kumpatia mwekezaji  ardhi,  matumizi,  na  muda  wa  mwekezaji  mgeni  kutumia  ardhi  hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...