Mwanasoka Bora Afrika Ndg. Mbwana Samatta akikabidhiwa baadhi ya zawadi mbalimbali na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir katika ofisi kuu za Bakwata zilizopo Kinondoni Jijini Dar Es Salaam. 
Leo tarehe 11 January 2016, Mwanasoka Bora Afrika Ndg. Mbwana Samatta alimtembelea Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir katika ofisi kuu za Bakwata zilizopo Kinondoni Jijini Dar Es Salaam.

Mufti Mkuu mbali na kumpatia zawadi mbalimbali kwa ajili ya kumsaidia katika imani yake pia alipata nafasi ya kumuombea dua ya mafanikio zaidi huko aendako Ulaya na kumpa nasaha asisahau kumuomba Mwenyezi Mungu kila wakati na kufanya ibada muda wote atakaokuwa nje ya mazoezi. 

Mwisho Mufti alimtakia mafanikio mema na kumuambia dua za watanzania wote zipo naye. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kila lijalo ni rizki ya Mola. Mbwana,umetuonesha njia bora ktk kuboresha imani, utanakuwa na mafanikio makubwa. Katika hili na jingine Mbwana dumisha imani yako na juhudi katika shughuli zako na kazi yako. Tunakutakia kila la kheri ktk mkataba wako mpya. Utakutana na changamoto mabalimbali katika safari hii ya maisha. Hizo ni kawaida,utayashinda yote na kufanikiwa zaidi, tuliza roho,ongeza bidii na ushirikiano. Katika hili umeonesha mfano mzuri wa kuigwa. La mwisho kutoka kwangu ni hili. Popote uendapo jitambue wewe na dini yako, Wazazi na ndugu zako, heshimu Serikali iliyopo na usiingilie familia za watu. Hii ni siri ya mafanikio. Kheir In Shaa Allah

    Mrs. B. Sam, Kanyamahela, Kibondo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...