Chama cha mapinduzi- Tawi la California, tunapenda kutoa salamu za pole zilizojaa masikitiko makubwa kwa familia na ndugu wa Marehemu wa Mwenyekiti wa Tawi la CCM la DMV Mzee George Sebo. 
Pia tunapenda kutoa pole kwa uongozi wa chama wa tawi la DMV kwa kuondokewa na kiongozi wao mahili. Lakini pia tunapenda kutoa pole kwa watanzania wote wa DMV na wengine wote waliomjua marehemu.
Tumesikitishwa na kuguswa sana na huu msiba hasa kwa kumjua marehemu kwa ukaribu sana, kwa mapenzi yake kwa watu wote na nchi yake. Wengi wetu huku northern California wanaccm na wasio wanaccm tunamjua marehemu kwa ukaribu kwani alikuwa akitutembelea huku mara kwa mara na kuna kipindi yeye na mke wake walikuwa wanachama wa jumuiya yetu ya watanzania waishio hapa bay area. 
Hivyo ni mtu wetu tunafahamu fika.
Kama chama tutamkumbuka sana kwa kuwa mzee wa ushauri katika chama chetu na matawi yetu hapa Marekani. Tutayazingatia yale yote aliyotuachia na kuyafanyia kazi.

Tunaomba mungu wa rehema aiweke 
roho yake mahala pema peponi. 
AMINA

Erick Byorwango

Karibu-Tawi la California.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...