Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuutaarifu Umma wa Watanzania
kuwa Uchaguzi wa Ubunge katika Jimbo la Kijitoupele – Zanzibar utafanyika
mnamo tarehe 20 Machi, 2016.
Uchaguzi wa Mbunge katika Jimbo la Kijitoupele - Zanzibar ni mojawapo
ya Majimbo yaliyoahirisha kufanya Uchaguzi tarehe 25 Oktoba, 2015 kutokana
na hitilafu kwenye Karatasi za Kura.
Aidha, Tume inapenda kuwataarifu Wananchi kuwa Watendaji (Msimamizi
wa Uchaguzi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi) walioteuliwa kipindi cha
Uchaguzi Mkuu wa 2015 ndio watakaosimamia na kufanya shughuli za Uchaguzi
huo. Uchaguzi huo wa Ubunge katika Jimbo la Kijitoupele hautakuwa na
Kampeni na Wagombea walioteuliwa kushiriki Uchaguzi ulioahirishwa mwezi
Oktoba, 2015 ndio watakaoshiriki Uchaguzi huu.
Vituo vilivyotumika katika Uchaguzi wa mwaka 2015 ndiyo
vitakavyotumika. Vituo vitafunguliwa saa 1.00 asubuhi na kufungwa saa 10.00
jioni. Watakaoruhusiwa Kupiga Kura tarehe 20/3/2016 ni wale ambao
wameandikishwa na majina yao yapo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura la
Kituo na waje na Kadi ya Mpiga Kura.
Imetolewa na,
Jaji (Mst.) Damian Z. Lubuva
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI
MWENYEKITI
26/01/2016



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...