Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mh. Luhaga Mpina amekiamuru kulipa faini kiwanda cha A to Z cha mjini Arusha , chenye kufanya kazi ya kuzalisha nguo na bidhaa za plastiki kutokana na ukiukwaji wa utekelezaji wa sheria namba 20 ya mwaka 2004 ya utekelezaji na usimamizi wa mazingira.
Mh Mpina alitoa agizo hilo jijini Arusha Jumamosi katika ziara yake ya kukagua usafi wa mazingira, kupanda miti na kutembelea viwanda,ambapo alibaini kuwa mnamo septemba mwaka 2015 kiwanda hicho kilipewa adhabu ya kulipa faini ya shilingi milionni 70 na kukaidi kufanya hivyo kwa kipindi cha miezi sita sasa.
Mh Mpina amekitaka kiwanda hicho kulipa faini hiyo kwa kipindi kisichopungua siku saba kinyume na hapo kiwanda hicho kitafungiwa.
Aidha Naibu Waziri Mpina alitembelea viwanda vya Sunflug na Lothia Steel vya jijini humo na kujione namna ambavyo vinakabiliana na utunzaji wa mazingira katika uzalishaji wao na changamoto ya kuzimikazimika kwa umeme jijini Arusha.
Mh. Mpina alikitaka kiwanda cha Chuma cha Lothra Steel kupima moshi unaotoka katika kiwanda hicho ili kujua kama una athari kwa mazingira na viumbe vinavyozunguka maeneo ya kiwanda hicho.
Ziara na Mh waziri katika jiji la Arusha ni matokeo ya utekelezaji wa agizo la Mh Rais John Pombe Magufuli la usafi wa mazingira unaotakiwa kufanyika kitaifa kila Jumamosi ya mwisho wa
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh Luhaga Mpina akiwa ziarani kukagua baadhi wa viwanda jijini Arusha Jumamosi.
(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
mwezi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...