SHIRIKA
LA UMEME TANZANIA (TANESCO)
MAELEZO
KUHUSU MRADI WA UMEME MBOPO TEGETA
DAR
ES SALAAM.
Februari 2, 2016 kwenye
blogi hii kuna mteja wetu kutoka Wilaya ya Kitanesco Tegeta alilamikia Shirika
kuchelewesha Mradi wa kupeleka umeme
eneo la Mbopo.
UKWELI NI KWAMBA: Mradi wa kupeleka umeme Mbopo unagharama
ya Tsh.236,396,581.73, na umegarimiwa na Shirika la Umeme Tanzania
(TANESCO) kwa asilimia 100.
UKUBWA WA MRADI: Mradi wa kupeleka umeme Mbopo unagharama
ya Tsh.236,396,581.73, na unagharamiwa na Shirika la umeme Tanzania
kwa ailimia 100. Mradi unahusisha;
- Ujenzi wa laini ya msongo wa kilovolti
33 yenye urefu wa kilomita 8 na nguzo 93
- Transfoma kubwa ya kusambaza umeme (100kva
33/0.4/0.23kv-01)
- Nguzo 62 za umeme wa msongo mdogo ya njia tatu yenye urefu wa kilomita 3.
KAZI ILIYOFANYIKA MPAKA
SASA:
- Nguzo zote 93 zimeshasimamishwa
- Waya zimevutwa kwa urefu wa kilomita 2
kutoka Mbopo zahanati hadi Pangaboy Bar.
SABABU ZA KUCHELEWA KWA
MRADI:
- Mradi huu umechelewa kukamilika
kutokana utaratibu wa manunuzi ya baadhi ya vifaa vya ujenzi kwenye mradi.
- Kukosekana kwa Njia ya kupitisha umeme (way leave) wakati wa zoezi la kusimamisha nguzo lilipoanza.
AHADI KWA WANANCHI:
Baada ya kupatikana kwa
vifaa hivyo, Shirika linategemea kuanza tena utekelezaji wa Mradi huu Jumatatu Februari
08, 2016 na kukamilika Februari 26, 2016.
MIRADI MINGINE MUHIMU:
Pamoja na mradi huu,
mkoa pia una miradi ambayo linategemea kujengwa kwa mwaka huu 2016. Taratibu za
kuwapata wankandarasi zinaendelea.
1. Mradi wa
kupeleka umeme Block 8 Mbweni Mpiji,
2. Mradi wa
kupeleka umeme Block 7 Mbeni Mpiji,
3. Mradi wa
kupelekea umeme Mbweni Teta,
4. Mradi wa
umeme Mabwe pande Kikwete Vision,
5. Mradi wa
kupeleka Umeme Kisauke
Uongozi unaendelea
kusisitiza kwa wateja wake kuwa Mipango mizuri na inayotekelezeka ya kuwapatia
watanzania umeme wa uhakika ipo na inaendelea kutekelezwa katika maeneo
mbalimbali nchini.
Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano,
TANESCO Makao Makuu.
Huku Malela Toangoma nako TANESCO wametelekeza nguzo na nyaya zaidi ya mwezi sasa.
ReplyDeleteVizuri sana. Na vipi kuhusu Goba???
ReplyDeleteMimi siye aliyeuliza swali la awali ambalo mmelitolea jibu hapa.