Katibu Mkuu wa Wizara ya
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel ameitumia salamu za Rambirambi
familia ya Mzee Dellan Tarmo kufuatia kifo cha kijana wao mpendwa Jovitha Dellan kilichotokea
kwa ajali ya gari mkoani Arusha juzi tarehe 31.1.2016.
“Pokea
rambirambi zangu za dhati, sote kwa pamoja tumepoteza kijana mchapakazi, hodari na aliyependa kushirikiana
na wenzake katika kazi zake, hakika tutamkumbuka siku zote” Katibu Mkuu amesema.
Katibu Mkuu, Pia amemtumia
salamu za pole kwa Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu(KBF)
na Wafanyakazi wote wa Bodi ya Filamu
Tanzania.
“Nimepokea
taarifa za kifo cha Jovitha Dellan kwa huzuni kubwa, najua machungu na maumivu
mliyonayo kwa kuondokewa na kiungo muhimu katika utendaji wenu, poleni
sana, niko nanyi katika msiba huu mzito
kwenu”, amesema
Katibu Mkuu huyo.
Katibu Mkuu amesema pamoja na
kwamba kifo hakiepukiki, bado ni kitu ambacho kinashtua, kuhuzunisha na kuleta
unyonge mkubwa kwa wafiwa katika jamii.
“Naungana nanyi katika kipindi hiki kigumu
kumuombea kijana wetu Jovitha Dellan ili mwenyezi Mungu ampe mapumziko mema ya
Milele” Mwenyezi Mungu awatie nguvu, awape uvumilivu
na subira katika kipindi hiki”.
“Niko
nanyi katika kipindi hiki kigumu kwa hali na mali, nawaomba msijisikie wapweke” Katibu Mkuu amesema na
kuwatakia utulivu na amani katika kipindi hiki cha msiba mkubwa kwa familia.
Marehemu Jovitha Dellan amefariki juzi tarehe 31 Januari, 2016 mkoani
Arusha ambapo alikuwa njiani kurejea kazini jijini Dar es salaam.
Marehemu
Jovitha Dellan anatarajiwa kuzikwa wiki hii mkoani Manyara.
Jovitha Dellan alikuwa ni Afisa
Utamaduni aliyekuwa akifanya kazi katika Bodi ya Filamu Tanzania iliyopo chini
ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Mungu ailaze Roho ya Marehemu
Jovitha Dellan mahali Pema Peponi - Amina.
Jovitha Dellan mahali Pema Peponi - Amina.
Imetolewa
na:
Idara ya
Habari(MAELEZO)
DSM.
2 Februari, 2016


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...