Baadhi ya Wadau wa Utalii wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii (hayupo pichani) alipokutana nao.
Waziri Maghembe akiwaeleza wamiliki wa kampuni zinazofanya shughuli za Utalii katika hifadhi ya Mlima Kilimanjaro ambapo aliwaeleza mambo mbali mbali yanayochangia kushusha pato la taifa .Miongoni mwa mambo aliyozungumza ni pamoja na kampuni za Utalii kutumia njia za Panya kupndisha wageni,Wapagazi kufa Mlima Kilimanjaro kutokana na baridi kali kwa kukosa mavazi maalumu ya baridi,Uchafu Mlima Kilimanjaro,Wageni kupatiwa huduma duni ,na mapunjo ya mishahara kwa wapagazi.
Mhifadhi Mkuu mpya wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) Betrita Loibooki akiwa katika kikao hicho ambapo alitamburishwa rasmi akichukua nafasi ya Erastus Lufunguro aliyehamishiwa Makao Makuu, Mhifadhi Loibooki alikuwa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Arusha (ANAPA).
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...