Mashimo wa Barabara eneo la soko la Mapinduzi kama panavyoonekana katikaka picha, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda leo jijini Dar es Salaam alipotembelea na kuagiza patengenezwe haraka iwezekanavyo.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akiangalia ubovu wa barabara ya Mwanachamala 'A' hadi Makumbusho jijini Dar es Salaam leo.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda amefanya ziara ya kukagua barabara ya Mwanayama 'A' hadi Makumbusho ambayo imeharibika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Akizungumza baada ya kukagua barabara hizo amewapa watendaji wa manispaa ya Kinondoni wiki mbili kushughulikia tatizo hilo kutokana na adha ya magari yanayotumia barabara hiyo.

Amesema kuwa kuharibika kwa barabara nyingi katika manispaa hiyo ni kutokana na kujenga chini ya kiwango.

Makonda amesema fedha zinatolewa kwa ajili ya ujenzi lakini baadhi ya watendaji wanajenga chini ya kiwango na kuwapa adhabu wananchi wanatumia barabara hiyo ikiwemo na gari za kubeba.

Aidha amesema kuwa watahakikisha barabara zinafanyiwa maboresho katika urahishaji wa usafiri katika Manispaa ya Kinondoni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...