Golikipa mahili wa Mbeya City Fc ya Mbeya, Juma Kaseja Juma (pichani) amerejea kikosini kutoa mapumziko ya majuma mawili aliyopewa na kocha Kinnah Phiri kufuatia mkewe Bi Nasra Nassor kujifungua watoto mapacha hivi karibuni.
Kwa mujibu wa mtandao rasmi wa mbeyacityfc.com Kaseja amesema kuwa amefurahi kusafiri na hatimaye kurudi salama kwenye timu yake huku pia akitoa shukurani zake za dhati wa wale wote ambao wamekuwa karibu nae yeye kama mchezaji na pia familia yake tangu alipojiunga na City.
“Nashukuru mungu nimefika hapa salama baada ya safari yangu, pia namshukuru kwa kile alichonijaalia, nimerudi kikosini nikiwa na ari kubwa zaidi ili kuituikia timu yangu kwa nguvu zote katika kutafuta mafanikio hasa kwenye kipindi hiki ambacho ligi inaelekea mwishoni, hakika tunapita kwenye kipindi kigumu lakini umoja wetu utatufanya kuvuka hapa” alisema.
Akiendelea zaidi Kaseja aliyewahi kucheza kwa mafanikio kwenye timu za Moro United, Simba, na Yanga aliweka wazi kuwa anaimani kuwa na kocha Kinnah Phiri kuwa ataijenga upya City na kuifanya kuwa timu itakayotisha zaidi kwenye msimu ujao wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...