Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP John Casmir Minja akisalimiana na Mkuu wa Kambi ya Utenganisho Mwisa, SP. S. Lubinza alipotembelea katika Kambi hiyo Machi 12, 2016 kisha kuongea na Wakimbizi kutoka Burundi ambao wanazuiliwa katika Kambi hiyo kwa mujibu wa Sheria.
Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP John Casmir Minja pamoja na ujumbe wake aliofuatana nao akikagua sehemu mbalimbali za Kambi hiyo ili kuona kama zinakidhi viwango vinavyokubalika katika kuwahifadhi Wakimbizi hao ambao wanahifadhiwa katika Kambi hiyo.
Askari Mlinzi kutoka Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza akiwa timamu kiulinzi kama anavyoonekana katika eneo lake la kazi ili kuhakikisha Ulinzi na Usalama wa Kambi hiyo Maalum iliyopo Mkoani Kagera.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...