Na Bashir Yakub.
Mtu anaposhtakiwa/kulalamikiwa hutakiwa kufika mahakamani. Lakini atafikaje mahakamani bila kujua kama ameshitakiwa. Ni lazima kuna utaratibu wa kumjuza mtu kuwa kuna shitaka dhidi yako. Na utaratibu ambao hutumika si mwingine bali ni kumtumia mtu wito maalum ambao hujulikana kama summons.
1.UTARATIBU WA SUMMONS KWA MAKUNDI MAALUM.
Wito au summons ya kuitwa kuhudhuria shauri baada ya kushitakiwa hutolewa kwa namna tofauti kutegemea na aina na mazingira aliyomo muitwaji. Upo utaratibu wa wa summons kwa mtu wa kawaida, utaratibu kwa mtu aliye nje ya nchi, utaratibu kwa mtu aliye nje ya wilaya au mkoa, utaratibu kwa watumishi wa vyombo vya ulinzi, utaratibu kwa mtu asiyejulikana alipo, n.k. Baadhi ya tofauti hizi ndizo zitakazotizamwa katika haya makala.
2. SUMMONS HUTOLEWA WAKATI GANI.
Summons/wito haitolewi tu wakati mtu anapofunguliwa shauri . Bali hutolewa hata kwa mashahidi, hutolewa kabla ya hukumu kwa yule ambaye hakuhudhuria kesi ambayo imesikilizwa upande mmoja, hutolewa kama ukumbusho kwa mtu ambaye alikuwa akihudhuria mahakamani lakini baade akaacha, n.k.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...