Watendaji wa Taasisi zilizochini
ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wakimpokea na kumkaribisha
kuanza kazi Ofisini kwake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali
Iddi baada ya kuteuliwa tena na Rais wa Zanzibar kuendelea kushika wadhifa huo
katika kipindi cha Pili cha Awamu ya Saba.
Katibu wa Makamu wa Pili wa
Rais wa Zanzibar Abdullah Ali Abdullah { Kitole } aliyeinama akinong’onezana
kitu na Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Ahmad
Kassim kwenye hafla ya kupokea Balozi Seif kuanza rasmi majukumu yake Vuga
Mjini Zanzibar.
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Ahmad Kassim akimpongeza Balozi Seif kutokana
na juhudi zake zilizopelekea watendaji wa ofisi yake kupata mafanikio makubwa
ndani ya kipindi cha uongozi wake wa miaka mitano iliyopita.
Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif akiwashukuru watendaji wa Taasisi zilizo chini ya Ofisi
yake baada ya kufanyakazi pamoja atika kipindi cha miaka mitano iliyopita.






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...