KUFUTWA USAJILI KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI (110) KWA KUJIENDESHA KINYUME CHA SHERIA KUANZIA TAREHE 30/03/2016.
Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali amefuta usajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiesrikali (NGOs) 109 kwa kuendesha shughuli zao kinyume cha Sheria ya NGOs Na. 24 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa mwaka 2005. Mashirika hayo ni yale ambayo hayajawasilisha taarifa za mwaka kwa kipindi cha miaka miwili pasipo kutoa sababu za msingi, kutolipa ada ya mwaka au kuendesha shughuli za NGOs bila kusajiliwa chini ya Sheria ya NGOs.
Kwa taarifa hii, Mashirika yaliyotajawa hapa chini yamefutiwa usajili na yataarifiwa kusitisha shughuli zao kuanzia tarehe ya tangazo hili (30/03/2016). Baada ya kipindi hicho, Msajili wa NGOs atayachukulia hatua stahiki Mashirika ambayo yatakaidi amri hii na kuendelea na shughuli za NGOs kinyume na Sheria husika.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...