Na Chalila Kibuda, Globu  ya Jamii.
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, amewateua wajumbe wanne wa kamati ya maudhui watakaotumikia kipindi cha miaka mitatu.

Taarifa iliyotolewa  leo kwa vyombo vya habari na Idara ya Habari Maelezo ilieleza kuwa uteuzi huo hufanyika kila baada ya miaka mitatu.

Wajumbe wa Kamati hiyo ni  Joseph Mapunda ambaye ni  mhariri Mtendaji Mstaafu wa Magazeti ya Serikali(TSN) na  Mkurugenzi Mstaafu wa Redio Tanzania Dar es Salaam(RTD) Abdul Ngalawa.

Wengine ni  Mwandishi wa habari ,Mhadhiri Derek Murusuri  pamoja na Mwandishi wa habari ,Mwanasheria , Zainabu Mwatawala.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...