SIMU.TV: Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Nape Nnauye atoa wito kwa viongozi wa dini nchini kutumia nyumba za ibada kuielimisha jamii kuondokana na imani potofu zinazo changia mauaji ya Albino na vikongwe.https://youtu.be/bDk5DjLDs8I
SIMU.TV: Mazishi ya baba wa katibu mkuu kiongozi balozi John Kijazi yafanyika leo nyumbani kwake wilayani Korogwe mkoani Tanga. https://youtu.be/M-0C4yQ4aRg
SIMU.TV: Wizara ya nishati na madini yatoa ufafanuzi kuhusu mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi linalotarajiwa kujengwa kutoka nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania. https://youtu.be/7nGm_X_3h20
SIMU.TV: Hatimaye shughuli za usindikaji wa ngozi katika ghala lililotajwa kuhatarisha afya za wakazi manispaa ya Dodoma zimesitishwa kufuatia agizo la Waziri Suleiman Jaffo. https://youtu.be/KdCeSVILNrg
SIMU.TV: Shirikisho la soka hapa nchini TFF limeaahidi kuwarudishia fedha mashabiki wote walionunua tiketi kuona mchezo kati ya Taifa stars na Chad baada ya timu ya taifa ya Chad kujiondoa kwenye michuano hiyo. https://youtu.be/XKm_0DXZ6Kw
SIMU.TV: Mshambuliaji Msweden Zlatan Ibrahimovich anayekipiga PSG amebainisha timu za Uingereza kumgombania ili aweze kuzitumikia msimu ujao.https://youtu.be/j3g5himL-gg
SIMU.TV: Katika hali ya kusikitisha watu 4 wapoteza maisha na wengine 38 kujeruhiwa baada ya basi kuacha njia na kupinduka mkoani Iringa. https://youtu.be/5xoOi4Uko8E
SIMU.TV: Askofu wa kanisa la AIC kanda ya Geita asema licha ya jitihada za kumbua majipu zinazoendelea iwapo watumishi wa umma hawatamgeukia Mwenyezi Mungu tatizo la rushwa na uhujumu uchumi vitaendelea tu. https://youtu.be/bv9sMH9PbVE
SIMU.TV: Jopo la wafanyabiashara 40 wa Tanzania katika sekta ya madini na nishati linatarajia kuondoka nchini kesho kwenda nchini Uganda kwenda kumshawishi Rais Mseveni kuipa Tanzania mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka nchini humo kuja Tanga. https://youtu.be/o8yVwZcgrlc
SIMU.TV: Rais John Magufuli apokea taarifa ya ukaguzi wa hesabu za serikali kutoka kwa mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali huku hafla hiyo ikihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali. https://youtu.be/ePZhJdhYDYs
SIMU.TV: Wachimbaji wa wadogo wa madini ya dhahabu walioko kata ya Kibindo mkoani Pwani wapinga hatua ya uongozi ya wilaya Bagamoyo kuwataka kuondoka katika machimbo yao kwa madai eneo hilo lina mwekezaji.https://youtu.be/gpLnieVzEyM


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...