Na Mwandishi Maalum, New York 
Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, kupitia Uwakilishi wake wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa, ni Mwenyekiti wa Kundi la Nchi za Afrika katika Umoja wa Mataifa kwa mwezi huu wa March. Miongoni mwa majukumu ya Mwenyekiti wa Mwenzi ni pamoja na kuitisha , kuratibu na kuendesha mikutano inayowahusisha Wawakilishi wa Kudumu kutoka Nchi 53 wanaoziwakilisha Nchi zao katika Umoja wa Mataifa. 
Mwenyekiti wa mwezi, pamoja na kuratibu na kuendesha mikutano yenye ajenda mbalimbali pia anawajibika katika kuwasilisha kauli ya nchi za Afrika kupitia ama utoaji wa hotuba au mawasiliano na Wakuu wa Idara mbalimbali ndani ya Sekretarieti ya Umoja wa Mataifa, akiwamo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa pale inapolazimu. 
Pichani ni baadhi ya Matukio yaliyotokea mwishoni wa wiki wakati wa Mkutano wa Wawakilishi hao wa Nchi za Afrika chini ya uenyekiti wa Tanzania, ambapo walipokea taarifa mbalimbali kutoka kwa watendaji wa Umoja wa Mataifa pamoja na taarifa kutoka kwa Muungano wa Wakuu wa Idara za Takwimu kutoka Afrika waliokuwa wakishiriki katika Mkutano wa 48 wa Kamisheni ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa.
 Balozi Tuvako Manongi akimkabidhi zawadi ya kumuanga  kwa niaba ya  Mabalozi wenzie  aliyekuwa  Mwakilishi wa  Kudumu wa  Liberia katika Umoja wa Mataifa, Balozi Marjon V. Kamara ambaye ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje  wa Liberia. 
 Mkurugenzi  Mkuu wa Ofisi  ya Taifa ya Takwimu, Dr. Albina Chuwa  (kushoto) akitoaa taarifa  fupi kwa niaba ya Wakurungezi  Wakuu wa Idara za Takwimu kutoka  Nchi za Afrika kuhusu maazimio na mapendekezo yao  kuhusu viashiria vya ajenda  ya Maendeleo Endelevu.  Kulia kwa Balozi Tuvako Manongi ambaye  Tanzania ni Mwenyekiti wa Mwezi wa  nchi za Kundi la Afrika ( African  Group) Ni Mtakwimu Mkuu kutoka Ivory Coast.
 Katibu Mkuu Msaidizi Mwandamizi wa Idara ya Siasa ya Umoja wa Mataifa, Bw. Taye-Brook Zerihoun  naye akiwasilisha taarifa yake kwa Wawakilishi wa Kudumu wa Nchi za Afrika, ambapo pamoja na mambo mengine aliwaomba wawakilishi hao kuunga mkono pendekezo la  Idara yake la kupatiwa fedha ambazo wanataka kuzitumia katika eneo la uratibu na usimamia wa majadiliano  kuhudu dhana  nzima ya uzuiaji wa machafuko ( mediation and  prevention ) pamoja na kuongeza ajira.
 Sehemu ya Mabalozi na Maafisa  kutoka   nchi Wanachamawa Umoja wa Afrika  wakifuatilia mkutano.
Sehemu ya Mabalozi na Maafisa  kutoka   nchi Wanachamawa Umoja wa Afrika  wakifuatilia mkutano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...