Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa, Hiiti  Sillo akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kukamatwa kwa kiwanda bubu cha kutengeneza perfumes bandia  aina SAME.leo  jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Hiiti  Sillo akiwaonesha wandishi wahabari (hawapo  pichani) mitambo ya kutengenezea perfumes bandia zinazoitwa kwa jina la SAME   leo jijini Dar es Salaam. 
Wandishi wakimsilkiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa, Hiiti  Sillo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA), Hiiti  Sillo akiwaonesha wandishi wa habari perfumes bandia zinazoitwa kwa jina la SAME   leo jijini Dar es Salaam.


 Na Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ,Kanda ya Mashariki kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi imekamata  vipodozi vya manukato ‘Perfume’  katika nyumba  inayomilikiwa na Mwanaidi iliyopo eneo la Tuangoma,  Wilayani Temeke Mkoani Dar es Salaam.

Akizungumzna na wandishi wa habari  jijini Dar es Salaam leo ,Mkurugenzi Mkuu wa TFDA,Hiiti Sillo amesema kuwa walipata taarifa juu ya utengenezaji wa mafuta ya manukato na ndipo wakafanyia kazi na kwenda kukamata.

 Amesema katika nyumba hiyo  ina vifaa vya kimaabara, malighafi na kemikali mbalimbali  za kutengeneza manukato yenye alama ya kibiashara  SAME huku mafuta yakionyeshwa stika kuwa inatengenezwa nchini Uturuki

Sillo amesema wangalizi wa nyumba hiyo Fatuma Selemani anashikiliwa na Jeshi la Polisi ili kusaidia upelelezi na jalada la Polisi na MBL/IR/1998/2016 limefunguliwa katika Kituo cha Polisi Wilaya ya Kipolisi Mbagala, Temeke.

Amesema vielelezo vyote ikiwa ni chupa 5,350 za perfumes zilizokamatwa dukani pamoja na vifaa, malighafi, kemikali na stika mbalimbali zilizokamatwa dukani vinashikiliwa.

Sllo  amewaomba wananchi wote ambao wanazo majumbani kwao perfumes aina ya SAME waache kuzitumia na wazirudishe katika ofisi za TFDA zilizopo hapa nchini kwa sababu perfumes hizo hazijasajiliwa na TFDA na hivyo ubora na usalama wake haufahamiki.

Aidha amesema wananchi waendelee kutoa taarifa kuhusu mtu au makundi ya watu mbalimbali wanaojihusisha na biashara haramu za utengenezaji, uzalishaji, usambazaji na uuzaji wa chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba katika maduka au majumbani mwao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...