Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bw. Casmir Kyuki akizungumza wakati wa makabidhiano ya Taarifa ya Utafiti wa Sheria ya Ununuzi wa Umma.
Mwenyekiti wa Tume Mhe. Jaji Aloysius Mujulizi akizungumza wakati wa makabidhiano ya Taarifa ya Utafiti wa Sheria ya Ununuzi wa Umma. Makabidhiano yalifanyika katika ukumbi wa Wizara ya Katiba na Sheria Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Mhe. Jaji Aloysius Mujulizi (Kushoto) akimkabidhi Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dk. Harison Mwakyembe Taarifa ya Utafiti wa Sheria ya Ununuzi wa Umma. Wengine pichani ni Katibu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sufini Mchome (wa pili kulia) na Katibu Mtendaji wa Tume Bw. Casmir Kyuki.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dk Harison Mwakyembe akiongea mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa makabidhiano ya Taarifa ya Utafiti wa Sheria ya Ununuzi wa Umma.
Sehemu ya Waandishi wa habari waliohudhuria makabidhiano ya Taarifa ya Utafiti wa Sheria ya Ununuzi wa Umma (Picha zote na Munir Shemweta wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania).


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...