Na  Bashir  Yakub.
Ipo  namna  nzuri  ya  umiliki  wa  ardhi  wa  pamoja  ambayo  huepusha  migogoro   hasa  kwa  walio  katika  ndoa. Migogoro  ya  ardhi  hutokea  kwa  namna  tofauti. Ipo  inayotokea  wakati  wa  uhai  wa  wamiliki  na  ile  itokeayo  baada  ya  uhai  wa wamiliki  wote  au  mmoja  wao . 

Umiliki  kwa  mafungu  yasiyogawanyika   huwa  ni  suluhu kwa  yote  haya. Ni  suluhu kwa  wanandoa  wenyewe  wanapogombea  mali  lakini  ni  suluhu wakati  ndugu  wanapotaka kumpokonya mwanandoa  ardhi  iliyoachwa  na  mwenza  wake baada  ya  kifo. 

 Ni  vema  kujua  kuwa sheria  ya  ardhi  kawaida  inatambua  umiliki  wa  ardhi  wa  aina  mbili.  Tumewahi  kueleza  umiliki  huo  hapa  lakini  leo  pia  tutaeleza.  Upo  umiliki  binafsi  na  umiliki  usio  binafsi  kwa  maana  ya  umiliki  wa  zaidi  ya  mtu  mmoja. 

1.UMILIKI  BINAFSI.
Umiliki  binafsi  ni  umiliki wa mtu mmoja. Kama  ni  nyumba, shamba  au  kiwanja  kinakuwa  chini  ya  jina  la  mtu  mmoja.  Huyo  mwenye  jina  linalosomeka  ndiye  huhesabika  kama  mmiliki  wa  pekee. 

Haki  zote zikiwemo  zile  za  kuhamisha, kuweka  rehani, kuuza, kugawa  humhusu  mtu  mmoja  pekee. Hahitaji  ridhaa ya  mtu  mwingine katika  kutekeleza   muamala  wowote  katika  umiliki  huu labda  yawepo  mazingira  maalum.

2.  UMILIKI  WA  PAMOJA .
Huu  ni  umiliki  wa  pamoja  kama  neno  lenyewe  lilivyo.  Kwa jina  la  kitaalam  hujulikana  kama   “co-occupancy”. Watu  wawili  au  zaidi  huweza  kumiliki  nyumba, shamba  au  kiwanja kwa  pamoja.  Haki  za  msingi  kama  zile  za  kuhamisha  umiliki, kuuza,  kuweka  rehani,kutoa zawadi   huwahusu  wamiliki  wote.
KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...