Leo Jumatano tarehe 30 Machi 2016 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala na Serikali za Mitaa chini ya Makamu Mwenyekiti Mh. Dkt.
Pudenciana Kikwembe walipata fursa ya kutembelea ofisi za MKURABITA kwa
ajili ya kujifunza juu ya madhumuni na shughuli za MKURABITA nchini.
Katika ziara hiyo walipokelewa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Utumishi
Mh. Angela Kairuki na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu Bw. Peter Ilomo
Aidha
walipokea taarifa fupi kuhusu MKURABITA na maendeleo ya shughuli za
urasimishaji nchini yaliyotolewa na Mratibu wa Mpango. Bi. Seraphia
Mgembe.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...