DR. FRANCIS MW. MSELLEMU
1941- 1996
Baba, Ni Miaka 20 sasa tangu uondoke hata bila ya kutuambia neno la KWAHERI!
Maisha yetu hayajawahi kuwa rahisi bila uwepo wako, Baba.
Japo watu wanatuona tukicheka , hawajui ni kiasi gani mioyo yetu inahuzunika kwa kukukosa malezi, mapenzi na uwepo wako wewe.
Hata hivyo tunamshukuru Mungu kwa kuendelea kutulinda, kututunza na kutubariki. Ameedelea kuwa kweli kwetu Mume wa Mjane na Baba wa Yatima.
Tunakuombea Pumziko la Milele, na tukiamini kwamba siku moja tutakutana na tutaimba Halleluya pamoja na wewe.
Unakumbukwa daima na Mke wako Mpendwa Kodawa Mikaline Msellemu - ‘Mama K’ kama ulivyo kuwa umezoea kumuita, Watoto, Wakwe zako, pamoja na Wajukuu. Ndugu , Jamaa na Marafiki nao hawajakusahau.
Pumzika kwa Amani DAD!
Umevipiga vita vilivyo vizuri mwendo umeumaliza imani umeilinda. Pumzika kwa amani ya Bwana baba yangu.
ReplyDelete