Ankal akiwa na  furaha na heshima kukutana na magwiji wa ndondi nchini Tanzania leo. Habibu Kinyogoli "Master" (kati) na Emmanuel Mlundwa "Mzee wa Ulaya" jijini Dar es salaam leo. 
-----------------------
Kwa wasiowafahamu Mlundwa alikuwa kwenye timu ya Tanzania ya Olympic mwaka 1980 huko Moscow, Urusi (BOFYA HAPA) ambako alifanya vyema. Mlundwa pia ndiye muasisi wa ndondi za kulipwa nchini 
Kinyogoli alinyakua medali ya shaba katika Olympic mwaka 1972 uzito wa wa Unyoya ama Featherweight (BOFYA HAPA) Mjini Munich, Ujerumani
Kinyogoli ndiye aliyekuwa bondia wa pili wa Tanzania kuleta medali ya mashindano yanayoshirikisha nchi kutoka nje ya Afrika Mashariki wakati alipopata medali ya fedha katika Michezo ya Pili ya Afrika (2nd All African Games) iliyofanyika mjini Lagos, Nigeria mwaka 1973.  
Hadi wakati huo mwanamasumbwi aliyekuwa ameleta medali kutoka nje ya mipaka ya Afrika Mashariki alikuwa marehemu Titus Simba, ambaye alipata medali ya kwanza ya fedha kwa Tanzania katika Michezo ya Jumuiya ya Madola mwaka 1970 huko Scotland. 
Miongoni mwa mabondia ambao ni matunda yake ni Majuto Mchevu, aliyemfundisha mwaka 1969  katika klabu ya Magomeni Community Centre, Zakaria Yombayomba, Habibu Mzungu, Bakari Selemani, Kweli Msigili, Abbas Pazi, Francis na nduguye Benedict Kakokele aliowafundisha mwaka 1971.
Mwaka 1973, aliweka historia nyingine kwa Tanzania baada ya kushiriki Michezo ya Pili ya Afrika nchini Nigeria. Katika robo fainali alimpiga bondia kutoka Madagascar na katika nusu fainali akamtwanga bondia kutoka Mali na kusonga mbele kwenye fainali kuwania ubingwa wa uzani wa Bantam, ambapo alikumbana na Omollo wa Uganda aliyemshinda Kinyogoli kwa pointi na hivyo Mtanzania huyo kuambulia medali ya fedha.

Katika klabu ya Urafiki mwaka 1973 aliwafundisha akina Charles Mhilu 'Spinks', Lazaro Makali, Salum Temianga, Herbert Sempoli na Mmasi, ambao walikuwa wakifanyia mazoezi Peninsula Hotel.

Baada ya kustaafu ndondi za ridhaa mwaka 1978 na kuanza kufundisha watoto ndipo alipopata nafasi ya kuwafundisha mabondia wengi zaidi. 
Mara tu baada ya kustaafu ndondi mwaka huo alianzisha klabu ya ndondi ya Simba na kwa kuanzia akawachukua watoto wa mzee Ally Matumla Namwera; akina Matumla, Haji, Rashid na Hassan, ambao hivi sasa wamekuwa maarufu katika mchezo huo duniani kote.

Baadaye akawachukua akina Mbwana, Karim na Mazimbo Matumla, Iraq Hudu, Joseph Marwa, Adeli Mkajanga, Oscar Manyuka, marehemu Steven Bicco, Patrick Kibona, Shabani Mhamila 'Star Boy' , Adam Abdulrahman, Maneno Oswald, Rajab Mhamila 'Super D' ambaye kwa sasa ni kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi na ni msaidizi wake katika kuwanoa vijana chipukizi kwa sasa, Abdallah Nyuni, Nassor Kondo, Rehema Matumla, Theresia Kapinga, na wengineo wengi.  

Enzi hizo mabondia nyota wa Afrika waliongozwa na Lottie Mwale na Francis Musankabala (Zambia), Steven Muchoki, David Attan, Michael Irungu, Robert Wangila, Isaya Ikonyi, na Modesti Napunyi (Kenya),

Wengine ni Emmanuel Mlundwa, Lucas Msomba, Ahmed Tesha, John Hugo, Clemence Chacha, Isangura, Nassor Michael, Joseph Marwa, Onesmo Ngowi, Gerald Isaac, Ali Muhamed, Emmanuel Kimaro, Rashid Matumla, Hamisi Kimanga na Koba Kimanga  (Tanzania), Ayub Kalule, John Mugabi, John Odhiambo, Boza Edward, John Byaruhanga,  Mustafa Waisaja  na Cuban Businge (Uganda).

Habibu Kinyogoli kulia aliyeshika kikombe na shingoni medali ya shaba akiwa na Waziri Mkuu na Makamu wa Rais wakati huo Mhe. Rashid Mfaume Kawawa  baada ya kutoka katika mashindano ya All African Game 1973 akiwa na bingwa wa riasdha Filbert Bayi aliyeshinda medali ya dhahabu kwa kuibuka mshindi wa kwanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...