Na  Bashir  Yakub
Baadhi  ya  wasomaji  wameuliza maswali  mengi  kuhusu  habari  ya  umiliki  wa  mali  kwa  wanandoa. Wanataka  kujua  ipi  mali  ya  ndoa  na  ipi  siyo, wanataka kujua   mali  unayokuwa  nayo  kabla  ya  ndoa  inahesabika  vipi  baada  ya  kuingia  nayo  katika ndoa, wanataka  kujua  uuzaji  wa  mali  za  ndoa,  wanataka  kujua  kigezo  kinachozingatiwa  katika  kugawana  mali ndoa  inapovunjika, wanataka  kujua  iwapo   inawezekana kuwa  na umiliki  wa  pekee  wa  mali   wakati  upo  katika  ndoa,  wanataka  kujua  haki  ya mali kwa  ndoa ya  mke  zaidi  ya  mmoja, wanataka  kujua  nani  kati  ya  mume  na  mke  ana  haki  zaidi  ya  mali  na  mengine  mengi.
Haya  yameulizwa  na  watu  tofauti  lakini  kwa  wingi. Hata hivyo mengi  yake  yalikwisha elezwa hapa.  Mengi  yameelezwa  katika  makala  tofauti zilizopita.  Tunaamini  wapo  walioona  na  wengine  hawakuona. Kwasababu  hiyo  hakuna  ubaya  kujibu  tena  maswali  ya  aina  hii  ili   hata ambao  hawakubahatika  kusoma  waweze  kusoma  leo.

1.JE  NDOA  INAPOVUNJIKA NI  KIGEZO  KIPI  HUTUMIKA  KATIKA  KUGAWA  MALI  ZA  WANANDOA.
Iliwahi  kuelezwa  hapa  kuwa  wengi  wanajua kuwa  katika  kugawana  mali  za  ndoa  pale  ndoa  inapovunjika  kigezo  kinachotumika  ni  cha  asilimia. Wanajua  kwamba  sheria  imeeleza  wazi  kuwa  kuna  asilimia  fulani  anatakiwa  kupata  mwanamke  na  asilimia  fulani  mwanaume.
 Hili  si  kweli  kwani  kigezo  kikubwa  kinachotumika  ni  kigezo  cha   nguvu au  juhudi  za  pamoja  katika  upatikanaji  mali( joint  effort) husika. Juhudi  za  pamoja  huangaliwa mchango  wa  kila  mmoja  katika  upatikanaji   au  uendelezaji  wa  mali  husika. 
Na  juhudi  za  pamoja  sio  tu pesa  au  mali  bali  pia  hata  kazi  za  nyumbani  nazo  ni  sehemu  ya  juhudi  za  pamoja  katika  kupatikana  kwa  mali.
Kwa hivyo  juhudi  ya kila  mmoja  itapimwa  na  mali  zitagawanywa. Mahakama  ndio  chombo  chenye  mamlaka  na  kazi hiyo.

KUSOMA  ZAIDI  NENDA sheriayakub.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...