Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa Vishale Tanzania (TADA), Subira Waziri akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani leo jijini Dar es salaam kuhusu kuanza kwa mashindano ya Afrika mashariki huku Tanzania ikiwa mwenyeji wa mashindano hayo kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Bi. Redempta Mwebesa.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mchezo wa Vishale Tanzania( TADA), Redempta Mwebesa (katikati) akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani leo jijini Dar es salaam kuhusu kuanza kwa mashindano ya Afrika mashariki , wa kwanza kulia ni Katibu mkuu wa chama hicho Bi. Subira Waziri na wa kwanza kushoto ni Afisa Habari wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bi Najaha Bakari.
Waandishi wa Habari wakifuatilia kwa makini mkutano
ulioandaliwa na viongozi wa Chama cha Mchezo wa Vishale Tanzania( TADA) hawapo
pichani kuzungumzia kuhusu kuanza kwa mashindano ya Afrika mashariki yanayotarajiwa kuanza April 29 mwaka huu.
Picha
na BMT.
Na Mwandishi wetu- BMT
MASHINDANO ya wazi ya Kitaifa na Kimataifa ya Shirikisho la Mchezo wa Vishale Afrika Mashariki yanatarajiwa kufanyika April 29 mpaka Mei Mosi jijini Dar es salaam, Tanzania ikiwa kama mwenyeji wa mashindano hayo.
Mashindano hayo yanatarajiwa kujumuisha nchi za ukanda wa Afrika mashariki zikiwemo Tanzania kama mwenyeji, Kenya, Uganda, Burundi na Ruanda huku Kenya ikiwa bingwa mtetezi wa michuano hiyo.
Akizungumza hayo leo jijini Dar es salaam Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa Vishale Tanzania (TADA) Bi. Subira Waziri amesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zitakazoshiriki michuano hiyo ikiwa na mategemeo makubwa ya ushindi.
“Tuna matarajio ya kuibuka washindi katika michuano hiyo kutokana na kujiandaa vya kutosha kwa upande wa mazoezi ukizingatia kuwa tuna utayari na uzoefu wa mchezo huo” alisema Waziri.
Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti wa TADA Bi. Redempta Mwebesi amesema kuwa licha ya mashindano hayo kuanza mwezi huu pia wana ukosefu wa Vifaa vya Michezo pamoja na gharama za kuweka kambi ili kujifua zaidi.
Aidha Bi. Mwebesi ameongeza kuwa wana ukosefu wa pesa taslimu na vikombe vya kuwapa washindi kwa kuwa wanategemea viingilio kutoka kwa washiriki wa mashindano hayo.
“Tunaomba wadhamini na wadau wa michezo wajitokeze kutusaidia kudhamini michuano hii kwa kutupa vifaa na gharama za kukaa kambini ili tuweze kujifua zaidi na kurudisha heshima tuliyoipata mwaka 2014 kwa kuibuka washindi wa michuano hii” aliongeza Bi. Mwebesa.
Pia Bi. Mwebesa ameongeza kuwa wana mikakati ya kuanzisha na kukuza mchezo huo kuanzia mashuleni , vijijini na Tanzania kwa ujumla ili kuweza kupanua na kuongeza ushindani wa mchezo huo nchini.
Na Mwandishi wetu- BMT
MASHINDANO ya wazi ya Kitaifa na Kimataifa ya Shirikisho la Mchezo wa Vishale Afrika Mashariki yanatarajiwa kufanyika April 29 mpaka Mei Mosi jijini Dar es salaam, Tanzania ikiwa kama mwenyeji wa mashindano hayo.
Mashindano hayo yanatarajiwa kujumuisha nchi za ukanda wa Afrika mashariki zikiwemo Tanzania kama mwenyeji, Kenya, Uganda, Burundi na Ruanda huku Kenya ikiwa bingwa mtetezi wa michuano hiyo.
Akizungumza hayo leo jijini Dar es salaam Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa Vishale Tanzania (TADA) Bi. Subira Waziri amesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zitakazoshiriki michuano hiyo ikiwa na mategemeo makubwa ya ushindi.
“Tuna matarajio ya kuibuka washindi katika michuano hiyo kutokana na kujiandaa vya kutosha kwa upande wa mazoezi ukizingatia kuwa tuna utayari na uzoefu wa mchezo huo” alisema Waziri.
Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti wa TADA Bi. Redempta Mwebesi amesema kuwa licha ya mashindano hayo kuanza mwezi huu pia wana ukosefu wa Vifaa vya Michezo pamoja na gharama za kuweka kambi ili kujifua zaidi.
Aidha Bi. Mwebesi ameongeza kuwa wana ukosefu wa pesa taslimu na vikombe vya kuwapa washindi kwa kuwa wanategemea viingilio kutoka kwa washiriki wa mashindano hayo.
“Tunaomba wadhamini na wadau wa michezo wajitokeze kutusaidia kudhamini michuano hii kwa kutupa vifaa na gharama za kukaa kambini ili tuweze kujifua zaidi na kurudisha heshima tuliyoipata mwaka 2014 kwa kuibuka washindi wa michuano hii” aliongeza Bi. Mwebesa.
Pia Bi. Mwebesa ameongeza kuwa wana mikakati ya kuanzisha na kukuza mchezo huo kuanzia mashuleni , vijijini na Tanzania kwa ujumla ili kuweza kupanua na kuongeza ushindani wa mchezo huo nchini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...