Sehemu ya wamiliki wa Kumbi za Starehe,Bendi na Wanamuziki wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda hayupo pichani leo jijini Dar es Salaam. (Picha na Emmanuel Massaka ,Globu ya Jamii.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiingia katika ukumbi wa Vijana leo kuwasilikiliza juu ya kilio wamiliki wa Kumbi za Starehe,Bendi na Wanamuziki juu ya agizo la kufunga kumbi hizo saa sita leo jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

WADAU wa Muziki na wamiliki wa bendi wamekutana kwa ajili kuangalia jinsi ya kuweza kuendesha shughuli zao kutokana na sheria ya muziki kufungwa saa sita.

Akizungumza na Wamiliki wa Bendi na Wanamuziki Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataka watu hao kuunda kamati ya kuona jinsi watavyoweza kubadili sheria kutokana na mazingira ya sasa.Makonda amesema kuwa Watu wenye bendi wanamchango mkubwa katika pato la taifa kutokana na vinywaji kunywewa katika kumbi hizo wakati bendi hizo zikifanya kazi.

Aidha amesema kuwa Mkoa wa Dar es Salaam kwa sasa watu wafuate sheria  na amri zikitolewa watu wakubali na sio kila mtu kuamuka kufanya yake pamoja na kuangalia haki ya mtu mmoja inayoadhiri watu wengine

Amesema katika watu wanaofanya biashara hiyo wanatakiwa kuangalia katika vipengele moja ni ya muda gani wa kufanya biashara ,wamiliki wa baa ni muda gani wanaweza kuanza , wapi watu bendi wanaweza kufanya muziki.

Makonda amesema kuna vitu vya kuangalia katika kufanya biashara hiyo kuwa ni sehemu gani watapiga na mazingira je kuna hospitali,shule ,kanisa, msikiti.Amesema kamati lazima iwe na majibu ya vitu ambavyo ni vya msingi katika kuendesha shughuli zao bila kuathiri watu wengine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...