Pichani ni vijana wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya Iringa Richard Kasesela (hayupo pichani).
Nafasi za kuingia JKT zimekuwa changamoto kubwa sana. Vijana Wilaya ya Iringa wamejitokeza zaidi ya vijana 612 kuomba nafasi za kujiunga na JKT. Nafasi zilizopo kwa wilaya nzima ni 100 tu. Zoezi la kusaili vijana linaendelea hadi jumatano. baadae Kamati ya Ulinzi na Usalama chini ya Mwenyekiti wake Richard Kasesela itakaa jumamosi kuchagua majina ya vijana hao. Mwitikio huu unaonyesha ipo haja ya kuongeza idadi inayotakiwa kwa vijana kwenda kwenye mafunzo ya hiari ya JKT.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...