Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani
Mwanza, Charles Kitwanga (aliyevaa koti) akishangiliwa na mamia ya wananchi wa
Kata ya Sumbugu wilayani Misungwi mara baada ya kuwasili katika eneo hilo kwa
ajili ya kufungua miradi ya maendeleo na kuzungumza na wananchi hao. Waziri
Kitwanga ameanza ziara jimboni humo leo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani
Mwanza, Charles Kitwanga (aliyevaa koti) akicheza ngoma ya Kisukuma iitwayo
Wachwechi wakati alipofanya ziara katika Kijiji cha Lutalutale, Kata ya Mbarika
jimboni humo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani
Mwanza, Charles Kitwanga akizungumza na wananchi wa Kata ya Mbarika jimboni
humo wakati kiongozi huyo alipofanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza
na wananchi katika kata hiyo.
Meneja
wa Utawala na Rasilimali Watu wa Mamlaka ya Maji Kahama na Shinyanga
(Kashwasa), Denis Mlingwa akimuonyesha Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye
pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi, Charles Kitwanga (kushoto) sehemu ya
kuchukulia dawa ya Kituo kipya cha Afya cha Ihelele jimboni humo
kinachotarajiwa kufunguliwa hivi karibuni kiweze kutoa huduma kwa wananchi wa
eneo hilo. Kituo hicho kitaongozwa na Kashwasa wakishirikiana na Halmashauri ya
Wilaya ya Misungwi.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani
Mwanza, Charles Kitwanga (kushoto) akimkabidhi mpira wa miguu Mwakilishi wa
Kitongoji cha Kashishi, Kata ya Sumbugu, Lucas Chai. Mbunge huyo alitoa mipira
ya miguu katika kata mbalimbali jimboni mwake. Picha zote na Felix Mwagara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...