Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Biashara na Viwanda wa Singapore, Dkt. Koh Poh Koon (kulia kwake) na ujumbe wake, Ofisini kwake bungeni mjini Dodoma Aprili 27, 2016. Kulia ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Biashara na Viwanda wa Singapore, Dkt. Koh Poh Koon (kulia ) na ujumbe wake kabla ya mazungumzo yao , Ofisini kwake bungeni mjini Dodoma Aprili 27, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Safi sana. Nafikiri kuna haja ya waziri wa viwanda kuandaa takwimu muhimu. Takwimu za mitaji. Ukitaka kuanzisha kiwanda hiki unahitaji mtaji wa shilingi kadhaa. Eneo liko sehemu fulani. Bank zilizotayari kutoa mikopo ni bank gani. Serikali inatoa upendeleo upi ili kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda. Watanzania wengi wanaogopa kumbe wanaweza. Serikali isaidie basi kufanya huo utafiti na kutoa takwimu. Tumeshuhudia Marekani ikishusha viwango vya riba ili kuhamasisha biashara. Tanzania vipi. Nafikiri tuko kwenye nafasi nzuri. Tufanye kitu cha ziada.
ReplyDelete