Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Bwana Sunil Colasso akiongea wakati wa kutambulisha Mr Money anayehakikishia wateja na watumiaji wa huduma za Airtel Money uhakika na gharama nafuu katika huduma za kifedha.

Airtel Tanzania imemtambulisha “Mr. Money” rafiki na mtoa habari njema atakayewasaidia wateja kutatua changamoto zao na kuwaelimisha kuhusu faida mbalimbali zinazotolewa kupitia huduma ya Airtel Money

Mr. Money ametengenezwa kuonyesha utofauti katika huduma za kifedha na kuondoa matabaka katika huduma tunazozitoa sokoni na kuzifanya ziwe zinafanana.

Mr. Money ataweza kuongea na watu katika umri tofauti vijana kwa wazee na kuleta uhai na thamani pindi wateja watakapotumia huduma zetu za kifedha. Kupitia mkakati huu mpya tunategemea huduma ya Airtel Money itakuwa zaidi

Akiongea wakati wa uzinduzi, Bwana Sunil Colaso, Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania alisema “Mr. Money atakuwa msaidizi ambaye atakusaidia kufanya mambo mengi zaidi kupitia huduma ya Airtel Money. atashughulikia changamoto zote na kutoa ufafanuzi juu ya faida mbalimbali zinazopatikana kupitia huduma ya Airtel Money na atasimamia mambo makuu mawili Uhakika na gharama nafuu katika huduma ya Airtel Money”.

Moja kati ya huduma za uhakika nafuu na zakibunifu zinazotolewa na Airtel Money ni pamoja na Mkopo ya Airtel Timiza, huduma hii ni mikopo isiyo na dhamana kwa wateja na mawakala wa Airtel Money ikifatiwa na Airtel Money Tap Tap pia ni huduma nyingine ya kibunifu inayotoa nafasi kwa wateja kufanya malipo kupitia kadi maalumu

Mr. Money ameshaanza kupasha habari njema kwa wateja wake kwa kuwawezesha wateja wake kupata Luku uniti za ziada pale wanaponunua LUKU kupitia Airtel Money, Mr. Money anaendelea na dhamira yake ya kutoa nyongeza ya ziada ya uniti za LUKU, na nyongeza za ziada za muda wa maongezi mteja atakapoongeza muda wa maongezi kupitia huduma ya Airtel Money, pamoja na kupata muda wa maongezi wa bure pale atakapotumia Airtel money kufanya malipo, kutuma pesa kwa wapendwa wao bure bila gharama yoyote na kuwawezesha wateja wake kufaidika kwa kiasi kikubwa na hivyo kuleta kutoa huduma zenye gharama nafuu zaidi sokoni

Usikose kupata habari njema kutoka kwa Mr Money kuanzia sasa kwani tunaamini kwa namna moja au nyingine zitabadili maisha yako.
kufurahia huduma mbalimbali zinazotolewa na Mr Money piga *150*60#

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...