Benki ya Exim Tanzania imeanza kukabidhi zawadi mbalimbali zikiwemo simu za mkononi na fulana kwa washindi wa kampeni ya benki hiyo inayoendelea ikihamasisha matumizi ya kituo chake cha huduma kwa wateja kwa njia ya mawasiliano ya simu.
Washindi wa kwanza wa benki hiyo walitangazwa mapema wiki hii mkoani Mwanza na kisha kukabidhiwa zawadi zao zilizoambatana na pongezi kutoka kwa uongozi wa benki hiyo tawi la Mwanza.
“Kwa sasa kupiga simu kwenye kituo chetu cha huduma kwa wateja humaanisha kupata msaada wa haraka kutoka kwa wahudumu wetu makini na pia ni kujiweka katika nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali zikiwemo simu za kisasa aina ya iPhone 5s,’’ alibainisha Meneja wa benki hiyo tawi la Mwanza, Bw Deogratias Makwaia wakati akikabidhi zawadi hizo, jijini Mwanza.
Kwa mujibu wa Bw Makwaia lengo la kampeni hiyo ni kuhamasisha matumizi ya kituo cha huduma kwa wateja wa benki hiyo kupitia namba ya simu 0784107600 huku pia wateja wakipata fursa ya kuwasiliana moja kwa moja na wahudumu wa benki ili kupata msaada na taarifa kuhusu huduma za benki hiyo.
“Bado watu wote wana nafasi ya kuendelea kushiriki kwenye kampeni hii na kujishindia zawadi zilizotajwa. Wanaweza kushiriki pia kwa kutembelea ukurasa wetu wa Facebook au kupiga simu kwa namba tajwa,’’ aliongeza
Wakizungumza baada ya kupokea zawadi zao baadhi ya washindi hao mbali na kuonyesha kufurahishwa na zawadi hizo walitoa wito kwa wateja wengine wa benki hiyo kushiriki kwenye kampeni hiyo.
“Nilifurahi sana nilipopokea simu kutoka Exim na kupewa taarifa kuwa nimejishindia simu aina ya iPhone 5s kwa kupiga tu simu huduma kwa wateja tena lengo likiwa na kupata msaada wa huduma ya kibenki…nilipatwa na mshtuko wa furaha,’’ alisema mmoja wa washindi hao Bw Chidiebere Abasirim.

Meneja wa benki ya Exim tawi la Mwanza, Bw Deogratias Makwaia (Kushoto) akikabidhi zawadi ya simu aina ya Iphone 5s kwa mmoja wa washindi wa kampeni ya benki hiyo inayoendelea ya kuhamasisha matumizi ya kituo chake cha huduma kwa wateja kwa njia ya mawasiliano ya simu wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa kwenye tawi la benki hiyo jijini Mwanza hivi karibuni.
Washindi wa kwanza wa benki hiyo walitangazwa mapema wiki hii mkoani Mwanza na kisha kukabidhiwa zawadi zao zilizoambatana na pongezi kutoka kwa uongozi wa benki hiyo tawi la Mwanza.
“Kwa sasa kupiga simu kwenye kituo chetu cha huduma kwa wateja humaanisha kupata msaada wa haraka kutoka kwa wahudumu wetu makini na pia ni kujiweka katika nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali zikiwemo simu za kisasa aina ya iPhone 5s,’’ alibainisha Meneja wa benki hiyo tawi la Mwanza, Bw Deogratias Makwaia wakati akikabidhi zawadi hizo, jijini Mwanza.
Kwa mujibu wa Bw Makwaia lengo la kampeni hiyo ni kuhamasisha matumizi ya kituo cha huduma kwa wateja wa benki hiyo kupitia namba ya simu 0784107600 huku pia wateja wakipata fursa ya kuwasiliana moja kwa moja na wahudumu wa benki ili kupata msaada na taarifa kuhusu huduma za benki hiyo.
“Bado watu wote wana nafasi ya kuendelea kushiriki kwenye kampeni hii na kujishindia zawadi zilizotajwa. Wanaweza kushiriki pia kwa kutembelea ukurasa wetu wa Facebook au kupiga simu kwa namba tajwa,’’ aliongeza
Wakizungumza baada ya kupokea zawadi zao baadhi ya washindi hao mbali na kuonyesha kufurahishwa na zawadi hizo walitoa wito kwa wateja wengine wa benki hiyo kushiriki kwenye kampeni hiyo.
“Nilifurahi sana nilipopokea simu kutoka Exim na kupewa taarifa kuwa nimejishindia simu aina ya iPhone 5s kwa kupiga tu simu huduma kwa wateja tena lengo likiwa na kupata msaada wa huduma ya kibenki…nilipatwa na mshtuko wa furaha,’’ alisema mmoja wa washindi hao Bw Chidiebere Abasirim.

Meneja wa benki ya Exim tawi la Mwanza, Bw Deogratias Makwaia (Kushoto) akikabidhi zawadi ya simu aina ya Iphone 5s kwa mmoja wa washindi wa kampeni ya benki hiyo inayoendelea ya kuhamasisha matumizi ya kituo chake cha huduma kwa wateja kwa njia ya mawasiliano ya simu wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa kwenye tawi la benki hiyo jijini Mwanza hivi karibuni.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...