RAIS Mstaafu wa awamu ya Pili, Alhaj Dk. Ally Hassan Mwinyi, amesema kuwa benki zimekuwa zikiendeshwa kwa kutoa mkopo bila riba hivyo itasaidia watanzania kujiwekea akiba na kuweza kukopa kwa ajili ya maendeleo yao .
Mwinyi ameyasema hayo leo , wakati akifungua kongamano la tatu la Taasisi za Kifedha za Kiislam Afrika, lenye lengo la kujengeana uwezo na wadau wa sekta za kifedha kwa watendaji linalofanyika kwenye hoteli ya Hyyat Regency kwa siku mbili katika kuwezesha urahisishaji wa usimamizi wa taasisi hizo na fursa ambazo wanaweza kuwekeza katika nchi za Afrika ikiwemo na Tanzania.
Amesema zipo baadhi ya benki zinatoza riba kubwa, hali inayowafanya wananchi baadhi ya wananchi kujiunga taasisi za kifedha na kuogopa kukopa mikopo kitokana na riba wanazotoza.Aidha amewawahamasisha wananchi kujiunga na benki za kiislaam ili kujiwekea akiba na kukopa fedha bila riba.
Nae Mkurugenzi wa Masoko kutoka Bima ya Kiislam Zanzibar, Said Abdallah, amesema asilimia 15 ya wananchi wanaojiunga na mfumo mpya wa bima ya Kiislam ni wapya.“Kuna umuhimu ya kuanzisha bima nyingine za kiislam nchini katika kuwezesha wananchi kujiunga na bima kwa ajili ya maisha yao,”amesema Rais Mstaafu, Mwinyi.Amesema pia sheria ya kuandaa bima za kiislam ni changamoto kubwa na kwamba hawajapata kibali kwa kamishina wa Bima tangu wameanza kufuatilia mwaka 2008 .
RAIS Mstaafu wa awamu ya Pili, Alhaj Dk. Ally Hassan Mwinyi akisoma hotuba yake wakati alipozindua kongamano la tatu la Taasisi za Kifedha za Kiislam Afrika, lenye lengo la kujengeana uwezo na wadau wa sekta za kifedha kwa watendaji wa taasisi hizo linalofanyika kwenye hoteli ya Hyyat Regency kwa siku mbili.
Baadhi ya wadau wakiwa katika Kongamano la tatu la Taasisi za Kifedha za Kiislam Afrika, lenye lengo la kujengeana uwezo na wadau wa sekta za kifedha kwa watendaji wa taasisi hizo.
Baadhi ya wasiriki wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo.
RAIS Mstaafu wa awamu ya Pili, Alhaj Dk. Ally Hassan Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kongamano hilo.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...