Baada ya kutikisa jiji la Dar es Salaam na manispaa ya Moshi leo Kampuni ya Bia ya Serengeti imeendelea kuwapa raha wateja wake kwa kuzindua promosheni ya Milioni 100 na Tusker- Fanya Kweli na Uwini Kanda ya ziwa ambapo Millioni 100 za Tusker Lager kushindaniwa. 

Uzinduzi huo uliofanyika jijini Mwanza Katika Bar ya Cross Park iliyopo Igoma wilayani Ilemela, ulipambwa na maonyesho ya barabarani ambapo msafara ulianzia Kiwanda cha Serengeti Igoma na kuishia Cross Pack Bar huku ukipokelewa na shamrashamra za aina mbalimbali.

 Promosheni hiyo itawapa fursa wateja kujishindia pesa taslimu Milioni 1 kwa washindi kumi (10) kila wiki kwa muda wa wiki kumi na kufanya jumla ya Milioni mia kushindaniwa na Zawadi za bia kibao. Promosheni hii ilizinduliwa rasmi na itaendeshwa kwa muda wa wiki kumi. Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wadau mbalimbali wa Kampuni hiyo pamoja na wana habari.

 Hii si mara ya kwanza kwa Kampuni ya Bia ya Serengeti kuendesha promosheni kama hii kwani ni wengi wameshanufaika kupitia promosheni mbalimbali za mfumo huu na hata kubadili maisha ya watumiaji wa bidhaa zake kwa kiasi kikubwa. Kupitia bia ya Tusker Lager Kampuni hiyo inaendeleza kile kilichokuwepo cha kurudisha fadhila na kutoa shukrani kwa watumiaji wa bia ya Tusker Lager.                 
Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Kanda ya Ziwa Patrick Kisaka akitoa maelezo ya promosheni hiyo kabla ya kuzindua rasmi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa promosheni ya Million 100 na tusker Fanya Kweli Uwini, iliyoandaliwa na kampuni hiyo jijini Mwanza.
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Kanda ya Ziwa wakicheza kufurahia uzinduzi wa Tusker Fanya Kweli Uwini jijini Mwanza.

Kikundi cha TYT kikitoa burudani wakati uzinduzi wa promosheni ya Million 100 na Tusker Fanya Kweli Uwini kanda ya ziwa uliofanyika jijini Mwanza -Cross Park Bar Igoma.
 
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...