Baada ya kutikisa jiji la Dar es Salaam
na manispaa ya Moshi leo Kampuni ya Bia ya Serengeti imeendelea kuwapa
raha wateja wake kwa kuzindua promosheni ya Milioni 100 na Tusker- Fanya
Kweli na Uwini Kanda ya ziwa ambapo Millioni 100 za Tusker Lager
kushindaniwa.
Uzinduzi
huo uliofanyika jijini Mwanza Katika Bar ya Cross Park iliyopo Igoma
wilayani Ilemela, ulipambwa na maonyesho ya barabarani ambapo msafara
ulianzia Kiwanda cha Serengeti Igoma na kuishia Cross Pack Bar huku
ukipokelewa na shamrashamra za aina mbalimbali.
Promosheni
hiyo itawapa fursa wateja kujishindia pesa taslimu Milioni 1 kwa
washindi kumi (10) kila wiki kwa muda wa wiki kumi na kufanya jumla ya
Milioni mia kushindaniwa na Zawadi za bia kibao. Promosheni hii
ilizinduliwa rasmi na itaendeshwa kwa muda wa wiki kumi. Uzinduzi huo
ulihudhuriwa na wadau mbalimbali wa Kampuni hiyo pamoja na wana habari.
Hii
si mara ya kwanza kwa Kampuni ya Bia ya Serengeti kuendesha promosheni
kama hii kwani ni wengi wameshanufaika kupitia promosheni mbalimbali za
mfumo huu na hata kubadili maisha ya watumiaji wa bidhaa zake kwa kiasi
kikubwa. Kupitia bia ya Tusker Lager Kampuni hiyo inaendeleza kile
kilichokuwepo cha kurudisha fadhila na kutoa shukrani kwa watumiaji wa
bia ya Tusker Lager.

Meneja
Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Kanda ya Ziwa Patrick Kisaka
akitoa maelezo ya promosheni hiyo kabla ya kuzindua rasmi wakati wa
hafla fupi ya uzinduzi wa promosheni ya Million 100 na tusker Fanya
Kweli Uwini, iliyoandaliwa na kampuni hiyo jijini Mwanza.

Baadhi
ya wafanyakazi wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Kanda ya Ziwa wakicheza
kufurahia uzinduzi wa Tusker Fanya Kweli Uwini jijini Mwanza.

Kikundi
cha TYT kikitoa burudani wakati uzinduzi wa promosheni ya Million 100
na Tusker Fanya Kweli Uwini kanda ya ziwa uliofanyika jijini Mwanza
-Cross Park Bar Igoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...