Miradi yote ya maendeleo nchini Tanzania kuhifadhiwa kwenye kanzi data ili kurahisisha uratibu, upembuzi, ufadhili na utekelezaji wake.Kituo cha kuchakata na kuzalisha umeme kwa njia ya gesi cha Kinyezi I kimekamilika kwa asilimia 88 na kinatarajiwa kuzalisha umeme kuanzia Septemba mwaka huu.

Akiongea katika ufungunzi wa mkutano wa kupata maoni ya taasisi za serikali zinazotekeleza miradi ya maendeleo, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Bi. Florance Mwanri alisema uwepo wa taarifa za miradi zitasadia taifa.

“Uwepo wa kanzi data hii utakuwa na manufaa sana kwa taifa kwa sababu itakuwa ni rahisi kufanya maamuzi katika mchakato mzima wa kutekeleza miradi” alisema Bi. Mwanri.

Miongoni mwa faida zitakazo tokana na mfumo huu ni kurahisisha upatikanaji wa vipaumbele vya miradi, kufanyika kwa upembuzi yakinifu vilevile upanikanaji wa fedha za kufadhili miradi hiyo. Pia mfumo huu utarahisisa utekelezaji na ufuatiliaji wa miradi iliyoidhinishwa na serikali.
 Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Bi. Florance Mwanri akifuatilia utangulizi wa  mapendekezo ya uundaji wa mfumo wa utunzaji wa miradi ya maendeleo – Kanzi data (Data Base), kushoto kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango Bw. Omar  Abdallah.
 Bi. Salome Kingdom akichukua taarifa za mapendekezo ya wadau mbalimbali ya kutoka taasisi za serikali ili kuboresha uundwaji wa wa kanzi data hiyo.
 Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakifuatilia mjadala.
 Kaimu Naibu Katibu Mtendaji – Uzalishaji, Bi. Lorah Madete, akielezea jinsi  taifa litakavyonufaika na mfumo huu. Kushoto kwake ni Bi. Zena Hussein na Bw. Hekima Chengula ambao ni sehemu ya kamati ya maandalizi.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Bi. Florance Mwanri akiteta jambo na wataalamu kutoka Tume ya Mipango kuhusu mrejesho wa mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...