Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii.
MASHINDANO ya Afrika kanda ya tano ya mpira wa Kikapu yamesogezwa mbele hadi Julai 19 kutokana na kukosa fedha za kuandaa mashindano hayo kwa sasa hadi pale bajeti ya serikali itakapopitisha mwaka mpya wa kifedha.
Mwenyekiti wa mashindano na katibu mkuu msaidizi Shirikisho la Mpira wa Kikapu nchini (BFT) Mwenze Kabinda amesema wamepokea taarifa hizo ila awali timu zimeshaanza kujiandaa kwa ajili ya michuano hiyo ya kanda ya tano Afrika.
"Tumepokea barua kutoka kwa katibu mkuu wa Kanda ya tano Afrika kutoka nchini Misri ikisena kuwa michuano hiyo itasogea mbele hadi julai 19 na kumalizika Julai 24,"amesema Kabinda.
Mashindano hayo yanakuwa ni kwa nchi za Kenya, Uganda, Tanzania, Burundi, Egypt, Eritrea, Ethiopia, Somalia Rwanda, Sudani na Sudan kusini.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...